Watu kadhaa wamenusurika kupoteza
maisha wilayani Biharamulo mkoani Kagera, baada ya basi walilokuwa wakisafiria
kugonga kundi la ng’ombe.
MACMEDIANEWS imezungumza na abiria wa basi hilo la Mohammed
Clasic likitokea Bukoba kuelekea mkoani Arusha, na kueleza kuwa ng’ombe 27
wameonekana kufa papo hapo kwenye ajali hiyo, huku akukuwa na abiria
aliyejeruhiwa wala kupoteza maisha kwasababu gari hilo alikuanguka.
Polisi wamefika kwenye eneo la tukio
kwenye moja ya kona za barabara kuu wilayani Biharamulo, na kuelekeza basi hiyo
namba T397 AMW kupelekwa kituo cha polisi kwa uchunguzi zaidi na utaratibu ili
wasafiri kuendelee na safari yao kwenda Arusha.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment