MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 16 July 2015

WAKATI MKUU WA MKOA AKITANGAZA MAPAMBANO, ACHINJWA MWINGINE BUKOBA.

. Asema kazi ya kupambana na wahalifu imeanza
. Mmoja atajwa kuchinjwa Kibeta


Wananchi wa mkoa wa Kagera wamehakikishiwa ulinzi na usalaama wakati wa maadhimisho ya siku kuu za Eid El Fitr ambazo zinatarajiwa kuadhimishwa mwishoni mwa wiki hii na Waislamu pamoja na wananchi wote nchini.

 Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. John Mongella wakati wa hafla ya kufuturisha iliyofanyika Ikulu ndongo mkoani hapa.
 
Amewatoa wasiwasi wananchi wa Bukoba juu ya vitendo viovu vya kukata makoromeo wananchi wasiyokuwa na hatia kuwa kwasasa wahalifu waliokuwa wanatekeleza vitendo hivyo wameanza kudhitiwa na mtandao mzima tayari umekamatwa na vyombo vya ulinzi na usalaama vinafanya kazi kuutokomeza.


Mhe. Mongella alisema hayo mara baada ya sala ya Magharibi tarehe 15/07/2015 na kuwasistiza waislamu wote pamoja na wananchi kuwa wasiwe na wasiwasi wowote juu ya ulinzi na usalaama wakati wa maadhimisho hayo. Pia alisema kuwa Kamati ya ulinzi na Usalaama imejipanga vizuri kuhakikisha maadhimisho hayo yanaadhimishwa katika hali ya amani na utulivu.



Akishukuru kwa niaba ya Waislamu na wanachi wengine waliohudhuria katika hafla hiyo ya futari  Sheikh wa Mkoa Aluna Kichwabuta alimshuru Mkuu wa Mkoa wa Kagera na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwakumbuka katika mfungo mtukufu wa ramadhani ambapo alisema hiyo ni ishara ya ushirikiano na undugu wa karibu kwao na serikali.

Aidha Sheikh Kichwabuta alikemea vitendo ambavyo vimeanza kujitokeza kwa wananchi kuvamia vituo vya Polisi kuvichoma au kupora siraha na kuwaua Maafisa wa Polisi ambapo alisema kuwa hiyo ni ishara mbaya na wananchi tunaanza kuhatarisha usalama wa nchi kwa kuanza kutekeleza vitendo hivyo viovu.


Sheikh Kichwabuta alikemea sana vitendo hivyo na kuomba sana wananchi wa mkoa wa Kagera wasijaribu kufanya vitendo hivyo viovu bali waendelee kudumisha amani na utulivu katika maeneo yao.


Mmoja atajwa kuchinjwa Kibeta

Wakati mkuu huyo wa mkoa na shkh wa mkoa wakikemea na kusisitiza kuanza kwa mapambano na wauaji, imetajwa kuwa kijana mwenye umri kati ya miaka 25-30 amechinjwa na kunyofolewa koromeo usiku wa kuamkia leo katika kata ya Kibeta manispaa ya Bukoba, ingawaje wiki mbili zilizopita, waziri wa mambo ya ndani Mathias Chikawe, aliueleza mtandao huu kuwa tayari amemuagiza DCI na ameshatua Kagera kwa uchunguzi zaidi.
Na Mwanaharakati.

No comments: