MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 16 February 2012

Kwanza hizi ni pikipiki kwa ajili ya kubebea mama wajawazito lakini kwa sasa hazijatumika na tayari ziko katika hali mbaya, yaani zimeanza kuhujumiwa kabla ya kazi.

 Hii ndiyo sura ya mbele ya Hospitali hii ya mkoa ikionekana safi kimazingira, lakini ndani kwenye WARD za wagonjwa kunatisha make mashuka ni machafu hasa katika vyumba vya waliojeruhiwa.

 Hiki juu ni kipande cha Shuka kimejaa dammu na nilipomhoji mama anaye muuguza mwanaye amesema damu hizo zina siku ya pili katika mashuka hayo, na hapa chini ni shuka Chakavu kwani limejaa matundu saidia wagonjwa hawa jamani.
 Mgonjwa huyu hapa chini amekaa hospitali zaidi ya wiki akisubiri upasuaji wa jicho baada ya kutoka chumba cha upasuaji amelazwa katika mashuka machafu yenye Damu.

 Ni Waziri katika ofisi ya rais Bwana KIDU MAKUBUYA pamoja na SYDA BBUMBA ambaye pia ni mbunge wa Nakaseke Kaskazini.
Maelezo zaidi kuhusu kilichosababisha utafahamu endelea kufuatili Mwanaharakati.
Wasiwasi wa mwanaharakati ni pale wanafuzi wanaposomea katika jengo ambalo halijakamilika, hii inamaanisha kuwa bora liende tuwe na hesabu ya shule lakini si kwamba wanafunzi wanapata cha kujifunza kwani hapo huwezi kukuta vitabu vya kutosha, walimu pamoja na mazingira bora ya kusomea, je mtoto anaweza kulinganishwa na yule anayesomea shule Kongwe?

Shule ya Kata Bugandika Kiziba inatumika kufundishia wanafunzi lakini bado haijakamilika, na hii ni kwasababu ya kuendeleza elimu hivyo wadau wa elimu jitokezeni kusaidia hali hii.
 Mpango huu wa upanuzi wa barabara katika manispaa ya Bukoba una lengo la kuanzia katika mzunguko (roundabout) Rwamishenye hadi Bandari kuu ya Bukoba KASTAM.
 Pamoja na ujenzi huo kuendelea kwa kusuasua, kuna sintofahamu inayowapa wasiwasi waliowengi ususani katika baadhi ya maeneo kwa walipoanzia upanuzi huu.

Ajabu ni pale wanapofikia kwa wale waliojenga kuingia barabareni wapanuzi hawa wanaweka kona kwa lengo la kuwakwepa kushhindwa kuwaondoa.
Huu ni mfano tosha katika eneo la Victorias ambapo packing ya magari iko kabisa barabarani sasa wajenzi hawa wameongeza kona upande wa pili kukwepa packing hiyo.
 Baada ya kuona Daraja au CARAVAT ya pale Annex kwa inakuwaje limefanywa finyu na kwanini upanuzi huu unaoneka sehemu zingine zimepanuliwa na zingine wanaziacha hivyohivyo? Kaimu meneja TANROADS Kagera Mhandisi Nasri Chakindo, alisema hayo ni mambo ya kiufundi ila nilipotaka kujua mambo gani hayo alisita kunena.
Upanuzi huu umenzia hospitali ya mkoa hadi Upendo ila zoezi litaendelea hadi kastamu na kule Rwamishenye kwani saizi hakuna fedha ya kutosha, hayo ni maneno ya TANROADS.

Tuesday 14 February 2012

 Ni mwaka mmoja na miezi miwili tangu mwangu pekee Bertha kuingia duniani hivyo pongezi za dhati sana na maisha marefu yenye Baraka namtakia kama babaake mpendwa.
 Ikiwa ni siku mwafaka ya wapendanao (VALENTINE DAY) mimi nimemzawadia ua maalum ndiyo maana kwa furaha naye kaamua kuniunga mkono kwa kulibusu.
Jah Bless you my Kid Bertha Lucky.

Monday 13 February 2012

 Ni kundi la waamuzi waliochezesha mechi kati ya Kagera Sugar na Mtibwa Sugar kutoka Morogoro.

 Baadhi ya wachezaji wa Kagera Sugar wakitoka uwanjani Kaitaba vichwa chini, baada ya kulazwa Bao 2-0, ndoto zao kupanda Ligi kuu Tanzania Bara zinafutika kwani mechi iliyopita katika uwanja wao wa nyumbani walipigwa bao 1-0 na JKT Ruvu.

Tuesday 7 February 2012


Pamoja na sheria za usalama barabarani kuzuia ujazaji wa abiria kupindukia, bado tatizo hilo ni sugu na linafanywa kwa makubaliano ya abiraia wenyewe.

Hili Basi la kampuni ya BUNDA BUS litokalo Mwanza Bukoba na Karagwe.
 HII NDIYO SHULE YA MSINGI KANGABUSHARO KATIKA KATA KARABAGAINE BUKOBA VIJIJINI.
 NI mwalimu mkuu wa shule ya Kangabusharo Bw. PILIUS EMMANUEL akiwa ofisini kwake shuleni hapo. Analalamikia kuwa na walimu wa kiume pekee katika shule hiyo ambapo wanashindwa kulifundisha darasa la saba kwasababu wanafunzi wa kike katika darasa hilo wengi wanabalehe hivyo kulifanya darasa hilo kuwa katika hali mbaya ya hewa na uchafu kwani wengi wanaingia katika siku zao EDHI bila kujijua hivyo kuwafanya walimu kuona aibu katika darasa hilo.
Hawa ni wanafunzi katika darasa la tano wanaonekana wadogowadogo lakini baadhi ya mabinti nao wakianza kubalehe inakuwa ni chnagamoto kwa walimu hao wakiume waliopo shuleni hapo.
Mwalimu PILIUS alipohojiwa nami amesema ameshapeleka maombi katika ofisi ya afisa elimu wa wilaya ya Bukoba kupatiwa walimu wa kike ila anashangaa kuona kimya.