MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday 26 July 2013

RAIS KIKWETE AZINDUA BARABARA YA KAGOMA RUSAUNGA MKOANI KAGERA

 Pamoja na uzinduzi huo, mh rais amesema kuwa serikali ina mpango wa kuanza msako mkali kwa majambazi yanayoteka magari na uvamizi mbalimbali, kuwa wanaomiliki silaha wazisalimishe ndani ya wiki mbili baada ya hapo majeshi yote nchini yanaanza msako na wanawahusika hawatakamatwa mateka.
 Juu ndiyo barabara iliyofunguliwa,

 Rais pia amepanda mti katika eneo la uzinduzi huliofanyika kwenye njia panda wilayani biharamulo.

 Mawaziri walioongoza na rais pia wameshiriki kupanda mti
 Kamanda wa polisi mkoanNI Kagera PHILIP KALANGI, akifuatilia ulinzi na usalama wakati wa uzinduzi na hotuba ya rais wilayani Biharamulo, na chini ni waziri wa ujenzi Dk Pombe magufuli akipinga ngoma ya Nyamigogo.
MWANA HARAKATI

Thursday 25 July 2013

RAIS KIKWETE AMEWAAHIDI WANANCHI WILAYANI MULEBA KUPIMA ARDHI NA KUONDOA MGOGORO KWA WANAOPAKANA NA KAMBI YA KABOYA.

 Mheshimiwa Mwijage, amesema kuwa mgogoro wa wananchi na kambi ya Kaboya, aueleweki kutokana na kutokuwapo mipaka ya kambi hiyo, kitendo kinachosababisha wananchi washindwe kutumia ardhi kutokana na masuala ya ulinzi na usalama, ilhali jeshi nalo linatakiwa kuheshimia.
 Katika hatua nyingine, mbunge huyo amesema kuwa wananchi wakabiliwa na ukosefu wa huduma ya umeme, ambapo walishapewa ahadi ya kupatiwa huduma hiyo kupitia REA, lakini hadi sasa hakuna kilichoishatekelezwa na kusababisha lawama kwa viongozi wa jimbo hilo.


 Rais Kikwete amesisitiza kuwa ulinzi na usalama umeimarika katika mkoa na nchi ya tanzania, kutokana na kauli ya mkuu wa majeshi Jenerali DAVIS MWAMUNYANGE, kuwahahikishia wananchi kuwa jeshi liko imara na linazingatia ulinzi kwa wananchi wake.
 Wananchi wakifuatilia hotuba fupi ya rais wa jamhuri ya muungano Tanzania baada ya kuweka dhana za asili kwenye mwenge wa kudumu ktk makaburi ya mashujaa.

Mbunge wa jimbo la Bukoba mjini Balozi HAMIS KAGASHEKI, akisalimiana na viongozi wengine wa kitaifa katika maadhimisho ya siku ya mashujaa kambini Kaboya.

Rais Kikwete ameendelea na ziara yake mkoani Kagera, ambapo sasa yupo wilayani Muleba ambapo atahutubia wananchi baada ya kuzindua mradi wa maji katika eneo la IYAKO, na bada ya hapo anapumzika na kuelekea Biharamulo.
MWANA HARAKATI

Wednesday 24 July 2013

RAIS KIKWETE AMEWEKA JIWE LA MSINGI KWEYE UWANJA WA NDEGE WA BUKOBA.

 Ris akivishwa bendera ya skauti
 Hii ni sehemu ya uwanja wa ndege wa Bukoba.
 Rais Kikwete akihutubia wananchi uwanjani hapo
 Mheshimiwa Kikwete akipewa taarifa na kusomewa ramani na mtaalamu wa ujenzi wa uwanja wa ndege
 Rais Kikwete akielekea kufungua pazia ya jiwe la msingi baada ya kukata utepe.
 Mheshimiwa Rais akisalimiana na baba Askofu Kilaini alipowasili uwanjani hapo
 Waziri wa maliasili na utalii Balozi Kagasheki, akibadilishana mawazo na waziri wa uchukuzi Arison Mwakeyembe na chini rais akihutubia wananchi baada ya kuzindua jengo la cha acha ushirika Kagera KCU.
 Chini ni picha ya pamoja na viongozi wa ushirika nyuma jengo hilo lililozinduliwa linaonekana kwa mbali.
MWANA HARAKATI

Tuesday 23 July 2013

UGANDA IMEWEKA UTARATIBU WA MACHINGA KUVAA SARE

 Ni kwa wafanyabiashara ndogondogo wanaouza vitu vidogovidogo kwa abiria kwenye stendi mbalimbali za magari.

 Hapa ni katikati ya jiji la KAMPALA, lilipomulikwa na kamera ya kandayaziwaleo ilipotembelea maeneo hayo.
 Wakati waganda wanaoonekana wakiuza ndizi, mishikaki na soda wakiwa na sare zao kwa mujibu wa utaratibu, Tanzania wao wanauza maziwa, karanga nk bila hata kuwa katika hali ya kuvutia wateja.



MWANA HARAKATI

MAANDALIZI YA SIKU YA MASHUJAA YAMEKAMILIKA VIWANJA VYA MASHUJAA KAMBINI KABOYA MKOANI KAGERA.

 Ni kikosi cha askari wa JWTZ kikitoka uwanjani baada ya kuigiza mapokezi na salamu ya rais ili kujiweka sawa.

 Makaburi ya walipolala makamanda waliopigania nchi na hapa chini ni upande wa makamanda wa Kikristo kama kibao kinavyoeleza.

 Ukaguzi wa rais ukiigizwa na viongozi waliokuwa katika viwanja hivyo kama wanavyotembezwa na uongozi kwa kutoa ufafanuzi kwa kiongozi.

 Baadhi ya magari yaliyofanya kazi wakati huo na sasa yamesalia kama magofu ila ni kionesho tosha.
 China unaona masalia ya magari, vifaru na bomu vilivyotumika enzi hizo.

 Ni viongozi mbalimbali wa kijeshi na dini akionekana kamanda wa polisi mkoa PHILP KALANGI.
MWANA HARAKATI

Monday 22 July 2013

JE RAIS KIKWETE ATAJIBU AU KUTEGUA KITENDAWILI CHA VIFO VISIVYOJULIKANA WILAYANI MULEBA?

 Mahojiano yangu mbalimbali usiku na mchana kujua hali hiyo ikoje, yamenifanya kugundua kuwa katika kata ya muhutwe wananchi wameshaamua kujifungia mapema kabla ya saa moja jioni wakihofia kutekwa.
 Kuhusu walichozungumza wananchi, wenyeviti wa kata na vijiji, kamanda wa polisi na mkuu wa wilaya ikibidi na mkuu wa mkoa wa Kagera, fuatailia vipindi vya redio Kasibante 88.5 MHz kupitia mboni ya jicho kila ijumaa 21:30 ni muda wa usiku na marudio jumapili saa 1 kamili jioni.
Pichani ni baadhi ya wananchi wakiwamo wenyeviti wa vijiji mbalimbali kwenye kata ua Muhutwe wilayani Muleba wakizungumza nami.
MWANA HARAKATI

SHULE YA SEMINARI YA KIISLAMU QDUS MJINI BUKOBA, YAFANYA HARAMBEE KUCHANGIA UJENZI WA BWENI NA MIUNDOMBINU MINGINE.

 Mbuh. Kagasheki amechangia sh milioni 5 na zingine 5 amewapa siku mbili lakini zilizosalia ili kukamilisha mil 23 za bweni, ambapo harambe imechangisha trip za mawe na sementi kutoka kwa wadau mbalimbali kutokana Kasibnte fm kurusha harambee hiyo iliyokuwa ikiendeshwa na waziri live. 
 Mgeni rasmi akisaini kitabu cha maudhurio.
 Mezani ni mil 5 alizotoa mbunge, huku akiendelea kuwata wadau mbalimbali walichangia kwa ahadi na cash.
 Haya ni baadhi ya majengo ya shule hiyo yenye wanafunzi 307 na walimu 26 ambao ni awali hadi drs la saba.

 Ni baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wakisikiliza kwa makini mazungumzo ya waziri Kagasheki.
MWANA HARAKATI

Friday 19 July 2013

SHIRIKA LINALOJISHUGHULISHA NA ELIMU YA UPATIKANAJI WA MAJI SALAMA SNV, LIMEPOKEA RIPOT YA WAANDISHI HABARI KUTOKA REDIO ZA KANDA YA ZIWA KUHUSU MRADI WA ELIMU YA MAJI KWA MWAKA MMOJA.

 Picha juu wa kwanza kushoto ni Mwanafunzi kutoka SAUT yupo SNV kwa field ya miezi3, wapili nyuma ni CONSOLATA TEM, cordinator SNV, wa tatu ni mwanahabari Mac Ngaiza kutoka Kasibante fm redio Bukoba, wa nne ni AYETA ambaye ni cordinator pia katika miradi ya SNV na amejikita katika ushauri kihabari, na mwisho ni mwanahabari kutoka redio FARAJA Shinyanga.
 Aliyesimama ni Projestus Binamungu wa Kasibante fm, akiwasilisha mada kwenye kikao cha wanahabari na SNV.
Mwanaharakati Nicolaus Mac Ngaiza ambaye pia ni mmiliki wa Blog hii, akiwa kwenye kivuko kimoja Busisi kwenye safari kuelekea Mwanza.
MWANA HARAKATI

WANAJAMII KUPITIA BLOG YENU HII, NIMEREJEA BAADA YA MICHAKATO MIREFU ILIYONIBANA KUWAPA HABARI, MSILAUHUMU BALI MNIOMBEE NIENDELEE NA KAZI YANGU HII YA KUHABARISHA.

Ni baada ya kutoonekana katika safu hii muhimu, katika kuweka habari, siyo kwamba nilifungwa, nilizuiliwa au niliacha kazi ya habari, bali nilikuwa na majukumu mengine muhimu ya kuongeza uelewa kichwani na kushidnwa kupata nafasi, leo nimerejea kwa nguvu mpya karibuni wadau.

MWANA HARAKATI