MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 31 October 2013

SIMBA v/s KAGERA LEO

Washabiki wa simba hii leo wamejipanga kuhakikisha timu yao inaibuka na ushindi, lakini kubwa zaidi uzalendo ni sehemu ya ushindi, je Kagera kupungua kwa mashabiki kunaweza kuikosesha ushindi?

MWANA HARAKATI

Tuesday 29 October 2013

ASKARI WATATU WA AKIBA (MGAMBO) WAMEKAMATWA KWA KUJIFANYA MAAFISA WA POLISI

 Hiyo ni baada ya mkuu wa mkoa wa Kagera kutangaza kuwa operation Kmbunga inaendela kuhusu wahamiaji haramu.
Wanamgambo MATHIAS SOSPETAR,MG 290305,ABED HAMAD(BABA AZU) MG436312 na AMRI SADICK MG436318 na aliyekimbia ni KATO MG 395092.Ambapo kamanda wa polisi mkoani Kagera amethibitisha kukamatwa kwao, na kusema kuwa baada ya kusikia zoezi linaendelea wameamua kuendelea pasipokuagizwa.
Walikamatwa Jumanne wiki iliyopita, lakini wamekaa rumande bila kufikishwa mahakamani, na taarifa zisizo rasmi wameachiliwa hatujajua km ni dhamana baada ya kutangaza taarifa zao.
MWANA HARAKATI

BIG RESULTS NOW.

Juu nikieleza kuhusu mpango wa tekeleza sasa kwa matokeo makubwa, miongoni mwa malalamiko ya wananchi katika manispaa ya Bukoba, kutoshirikishwa kwao anglau kupitia mikutano, kutopata mrejesho wa miradi wanayoibua, viongozi ngazi za kata kuchanganya mambo ya siasa na kitaalamu.
 Juu ni mtendaji kata Kashai, ambapo kumejitokeza miundombinu mibovu ya barabara, kufanyika miadhala na burudani katika maeneo ya shule wakati wa masomo, na uwingi wa wanafunzi wakati shule ni chache.
 Juu na chini katika shule ya sekondari Buhembe, ambapo mdahalo umefanyika na kuibua wanafunzi kupungua kila mwaka kuanzia 2007 ilipokuwa na wanafunzi 351 na sasa 227 kutokana na kuhamishwa kwa viongozi mara kwa mara, ambapo kila uongozi unaleta taratibu zake ikiwamo kubadili sare za shule kila anapoingia mpya, jambo lingine wazazi kutochangia gharama za masomo za mwanafunzi.
 Chini ni kata Kitendaguro, wao wanasema wamechoshwa na kutangaziwa miradi hewa.

Vipindi kuhusu BIG RESULTS NOW vitaanza kurushwa kupitia redio za kanda ya ziwa ikiwamo Radio yangu Kasibante fm kuanzia ijumaa wiki hii, sikiliza mawazo ya wananchi na viongozi wao ana kwa ana. 
MWANA HARAKATI

Sunday 27 October 2013

MATOKEO YA UCHAGUZI TFF MALINZI NA NYAMLAN 50-50

Wakati wanahabari wakizuiliwa kuingia kwenye chumba cha kupigia kura, taarifa za sasa zinasema kuwa inaonekana wanaouchuana katika kinyang'anyiro cha urais wa TFF, wanalingana kutokana na wadau na wapiga kura waliokuwa wakizungumzia pande zote mbili.

Bado tunafatilia taarifa kwani mpaka sasa wanahabari tupo nje kutokana na kuzuiliwa kuingia ndani ya chumba cha mkutano.

MWANA HARAKATI

ROCK CITY MARATHON



MWANA HARAKATI

Sunday 20 October 2013

JULIUS NYAISANGA AFARIKI DUNIA

 
Mpaka mauti yanamfika, Marehemu Nyaisangah alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Abood Media iliyopo mkoani Morogoro.
Marehemu aliwahi pia kufanya kazi katika kituo cha Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) na katika Kituo cha Redio One ambapo alikuwa Mkurugenzi.
Mpaka sasa chanzo cha kifo chake bado hakijafahamika japo marehemu alikuwa akiugua kwa muda mrefu.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMEN!  Taarifa zaidi zitawajia baadaye.
Marehemu Julius Nyaisangah (katikati) akiwa katika pozi na Meneja Mkuu wa Global Publishers Abdallah Mrisho katika semina ya wanahabari Bagamoyo mwaka 2011.
MWANA HARAKATI

Friday 4 October 2013

WASHINGTON DC

President Barack Obama demanded an end to a three-day government shutdown he decried as a reckless "farce," piling pressure on Republicans to climb down first on a budget impasse.
The US Treasury meanwhile warned of "catastrophic" consequences if there is no deal within weeks to raise the country's debt ceiling, and the IMF chief said navigating a way out of that next crisis was "mission critical."
Obama traveled to the Washington suburbs to lambast Republican House Speaker John Boehner, who emerged from a White House meeting late on Wednesday complaining that the president would not negotiate with him.
MWANA HARAKATI