MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday 29 November 2014

MWISHOWE BUNGE LAAZIMIA HAYA HAPA WAHUSIKA KUYIMULIWA

Ni baada ya maazimio mapya ambayo yamepitishwa na bunge kuwa wahusika wote uteuzi wao uangaliwe na kutenguliwa.

Wamo waziri wa nishati, waziri wa aridhi nyumba na Makaazi, mwanasheria mkuu na katibu wa wizara ya nishati na madini.

Hatahivyo bunge limeadhimia mikataba kurejerewa huku mitambo ya I PTL kutaifishwa ili kuhudumia watanzania.
Na Mwanaharakati.

BREAKING NEWS! RAIS KIKWETE AGOMA KUZUNGUMZIA ESCROW BAADA YA KUWAAILI UWANJAWA WA NDEGE DAR.

Pamoja na kuwapo subira kuwa atazungumzia kinachoendelea kuhusu ESCROW huko Bungeni Dodoma, Rais Kikwete bado anaendelea kuelezea kuhusu ugonjwa aliokuwa akitibiwa kwakutaja kuwa madaktari waligundua sehemu ya kansa katika vipimo14 walivyochambua kwenye tezi hilo dude.

Amehitimisha mazungumzo yake kwakusisitiza kuwa hagusii kinachojiri Dodoma kuwa hakijui vizuri na akikijua atasema.
Na Mwanaharakati.

Friday 28 November 2014

BREAKING NEWS BUNGE LAVUNJIKA WAPINZANI WAPINGA KUTONG'OKA KWA WATUHUMIWA

spika Makinda amelazimika kuahirisha bunge hilo ikiwa ni saa tano kasoro dk 20 baada ya kambi ya upinzani kuonesha wasiwasi katika maazimio yanayopitishwa baada ya baadhi ya wabunge kumtetea waziri wa nishati huku mwanasheria mkuu akikiri kuwa alikosea hivyo ashughulikiwe yeye badala ya katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini.

Bi Makinda ametoa muda usiojulikana kutejea kwa bunge kuendelea na mandala wa maazimio.
Na Mwanaharakati.

BREAKING NEWS!!! KAFARA BUNGENI

Ni aidha waziri wa nishati na madini profesa Sospeter Muhongo au mwanasheria mkuu wa serikali Frederick werema ambaye amepewa nafasi kujieleza na anaendelea kujieleza hivi Sasa.

Hali isiyo ya kawaida imejitokeza baada ya viongozi muhimu katika CCM Stephen Wasira , Mac  Mwandosya na Mwigulu November, kuwabana katika mgogoro wa ESCROW na kuwataka wajipime haraka huku wakitakiwa kutekeleza watakayoambiwa muda si mrefu.
Na Mwanaharakati.

TETESI ZA AFISA TRA KUFUKUZWA, HUKU BUNGE LA AHIRISHWA, WABUNGE WAKITAKA WAHUSIKA KUTUA MZINGO BILA KUWACHELEWESHA

Katika kikao cha leo, wachangiaji wa mjadala kuhusu ESCROW wamesema kuwa kuna kila sababu ya kutazama hali ya wananchi hasa baada ya kuona mali yao ikitafunwa na baadhi ya watanzania wenzao.



Tetesi inasema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Fedha imemfukuza kazi afisa wake wa TRA Plasidus Luoga kutokana na kuwa mmoja wa watu wanaotajwa chukuwa pesa za Escrow.

Inatajwa kuwa Plasidus Luoga,aliwekewa kiasi cha Milioni 121.2 kwenye akaunti yake Mkombozi Benki.




Na Mwanaharakati.

TANZANIA HAS NEVER HAD ANY PLAN TO EVICT THE MAASAI PEOPLE FROM THEIR ANCESTRAL LAND



DAR ES SALAAM, Tanzania, November 28, 2014/ -- The government of United Republic of Tanzania has never had any plan to evict the Maasai people from their ancestral land as falsely reported by the media in recent days. The information circulated through the media outlets globally was misleading, malicious and meant to tarnish the image of our country and her international standing.



The Minister of Natural Resources and Tourism (http://www.mnrt.go.tz), Hon. Lazaro Nyalandu said that the claims that 40,000 Maasai were being evicted are false unfounded and baseless. The argument that the land in question is being sold to a wealthy Middle Eastern family are a total fabrication and in contrary to the Tanzanian law.
Members of Parliamentary Standing Committee on Land, Natural Resource, and Environment are due to visit the Loliondo area to bear witness to the government position and speak directly to the Maasai people. The Minister, Lazaro Nyalandu will also be leading a team of government officials and Media Houses to visit Ngorongoro in the next few days.
Lazaro Nyalandu (MP)
Minister for Natural Resources and Tourism
28th November, 2014

Na Mwanaharakati.

BONGO MOVIE-SIFA HIZI ZA KWELI?

MSANII wa vichekesho (komedy) kutoka Nigeria,Okopcha Bright Onyekere maarufu kama Basket Mouth amewasifu wasanii wa Tanzania kwa juhudi wanazofanya kuelimisha jamii kutumia vipaji vyao.
Akizungumza Dar es Salaam jana baada ya kuwasili kutoka Nigeria kwa ajili ya onesho maalum kushirikiana na wasanii wa Tanzania juzi Dar es Salaam alisema kutoka aanze sanaa ya vichekesho miaka 16 iliyopita amekuwa akipata sifa za wasanii wa Tanzania wakiwika katika fani za muziki, sanaa za filamu, michezo ya kuigiza na vichekesho.

Onyekere aliyetamba nchini Nigeria na Bara la Afrika katika fani hiyo amekuja kufanya onesho moja lililopangwa kufanyika jana hoteli ya Golden Tulip, aliongeza kuwa sanaa ni utajiri mkubwa kama vipaji walivyopewa vitatumika ipasavyo na kutawala jukwaa .


Mkurugenzi wa Kampuni ya Vuvuzela, Evans Bukuku alisema lengo la kumleta msanii huyo wa komedy ni kuimarisha sanaa ya vichekesho kwa wasanii chipukizi wa Tanzania ambao wanahitaji kuandaliwa kwa soko hilo nchini na nje ya nchi.

Alisema Kampuni ya Vuvuzela imejitolea kusaidia wasanii wa vichekesho nchini na kuwafundisha namna watakavyoweza kuendeleza fani hiyo kazi iliyoanza miaka minne iliyopita kampuni ilipoanzishwa.

Bukuku alisema kila mwisho wa mwezi kuna onesho maalum ambalo hutumika kuonesha vipaji vya wasanii wa vichekesho na jinsi msanii anavyoweza kutawala jukwaa kuwaburudisha watazamaji.

Alisema kampuni yake inatarajia kufanya maonesho kama hayo mikoa mbalimbali ya Tanzania kuibua wasanii wengine wenye uwezio katika fani hiyo.

Mkurugenzi Bukuku alisema katika onesho la karibuni Watanzania walikongwa nyoyo zao pale wasanii wa Tanzania washirikiana na wasanii wa vichekesho kutoka Kenya ambaye ni Mdomo Baggy na Dick Omondi kutoka Uganda anayejulikana kama Uncle Bob kufanya onesho kali nchini.

Bukuku aliwashukuru wadhamini waliojitokeza kusaidia kufanyika kwa onesho hilo ambao ni Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA),Hoteli ya  Golden Tulip, Gazeti la Mwananchi Communications, Clouds Media Group, Ultimate security, Simu TV, Prime Advertising, Dar insites, Advertising Dar, Bongo 5, Eventlites, Hugo Domingo na Michuzi Blog.


Na Mwanaharakati.

WAWEKEZAJI WAVUTWA GEITA



Na Valence Robert Geita.
28.11.2014.
WAWEKEZAJI Mkoani Geita  wametakiwa kuwekeza kwa  wingi kwenye  Mkoa huo ili  vijana  walioko kuweza kupata ajira  kuliko kwenda kuwekeza kwingine na kuwanufaisha wasiokuwa wazawa wa Mkoa husika.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Geita Manzie Mangochie wakati wa kufungua KG Hotell iliyoko katika  mtaa wa misheni  kata ya kalangalala Wiyani Geita Mkoani hapa iliyojengwa na mfanyabiashara mzawa.

Mangochie alisema kuwa wafanyabiashara  Mkoani Geita wamekuwa wakienda kuwekeza Mikoa mingine au nchi za nje na kuwanyima haki ya kupata ajira vijana wazawa hivyo kuwaomba kuendelea kuwekeza katika mkoa huwo  ili na maendeleo yazidi kukua kwa kasi.

Jamani nawaomba wafanyabishara wa Mkoa huu muwekeze katika Mkoa huu ili vijana wetu waweze kupata ajira kuliko kuwekeza kwingine na ninawaomba kuzingatia kama kazi uliyo nayo inaweza kufanywa na watu wa Mkoa huu sioni haja ya kwenda kutafuta kwingine maana kuwapa ajira wazawa nanyi mnaongezewa zaidi alisema Mgochie.


Na Mwanaharakati.