MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday 19 October 2011

                                                            PORINI BUZIKU(CHATO)
Kumekuwa na taratibu za kukataza ukataji wa mkaa katika misitu ya hifadhi mkoani kagera lakini wakti huo mkoa huu ukiwa ni ule unaoongoza kuwa na gharama kubwa katika upatikanaji wa nishati mbadala.

Buziku ni moja ya misitu ya hifadhi ambayo imehifadhiwa kwa ajili ya mimea kitaifa lakini kwasasa ni sehmu ambayo imeshambuliwa na ukataji wa mkaa kwa kiasi kikubwa pamoja na uchungaji wa mifugo na kilimo katika msitu huo.

Kwenye picha huo ni baadhi ya magunia ya mkaa ambayo yameshuhudiwa na mtaalamu wa habari hizi wakti huo akiongea na wahusika wakasema kuwa wanafanya hivyo kwasababu ya maisha magumu.

Kwaupande wake afisa mali asli wa wilaya ya Chato bwana CHARLES SALEHE anasema msitu unapunguwa kwa kiasi kikubwa lakini wao kama wahusika wanakabiliwa na vitendea kazi ili kufanya doria za kutosha na baadhi ya wanasiasa wanahusika kuwadanganya wavamizi hao kwa kisingizio cha kuwapigia kura.
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM kata kagondo IGNATUS SIMON amekuta kondoo wake wanne wamechinjwa usiku wa kuamkia leo 19/10/2011 nyumbani kwake Kagondo karuguru katika manispaa ya Bukoba.

Akiongea na mwandishi habari hizi leo asubuhi mwenyekiti huyo amesema baada ya kuamka leo saa moja amekuta wamechinjwa pembezoni mwa zizi la kondoo hao wanne ambapo pia kilichomshangaza kutokuona damu zilizomwagika.

Akifafanua katika hilo amesema ametoa taarifa kituo cha polisi mjini Bukoba ambapo katika maelezo yake hakusita kueleza ugomvi alionao kwa jirani yake ambaye hakupenda kumtaja jina lakini akasema kuwa wamekuwa wakirumbana kwasababu za kisiasa na wakti huo pia wanagombea shamba ambapo kesi yao iko mahakamani.

Kondoo hao wamechinjwa usiku wa kuamkia leo siku ambayo walitarajia kumpeleka mwanasheria ili kukagua eneo linalogombewa hivyo alipofika naye ameshuudia hali hiyo.

Ripoti yake polisi ameitoa na kupewa RB NAMBA BU/RB/5619/2011.

Friday 14 October 2011

 Ujenzi holela unaoendelea kufanywa na wananchi wenye pesa zao katika manispaa ya Bukoba unasababisha maafa pamoja na kuharibu shughuli za maendeleo kwa baadhi ya watu na wakti mwingine kusasabisha maji kufunika madaraja ya mto kanoni ambayo hutumiwa na wananchi kupita kwa ajili ya shughuli zao za kila siku.

Pichani ni eneo linalopakana na hotel ya PRINCE mjini Bukoba ambpo kumefanyika ujenzi huo holela na kubadili mkondo wa mto kanoni ambo utokea kata za kagondo na nyanga ukikatiza katikati ya mji na kumwaga maji yake ziwa victoria.

Kutokana na ujenzi huu habari za uhakika kuhusu wanaotoa ruhusa ya watu hawa kujenga zinashindwa kudhibitishwa kwani wahusika wa halmashauri wanadai kuwa wananchi wanaamua kukaidi taratibu lakini kwa upande wa wajenzi wenyewe wanadai wamepewa hati za umiliki wa ardhi hvyo wana ruksa ya kujenga maeneo hayo.

Mvua zinapoanza kunyesha mkoani kagera manispaa inaathirika kwani baadhi ya makazi ya watu kama MUKIGUSHA maji uingia hadi ndani ya nyumba zao, kwingine biashara usimama kama inavyoonekana katika picha hapa chini.
Ni vibanda vya wafanyabiashara vimezingirwa na maji na shughuli zimesimama katika eneo la    PEDESTRIAN BRIDGE kanoni baada ya mvua iliyonyesha leo  Tarehe 14/10/2011.                  
MAKAMU WA RAIS MOHAMMED GHARIB BILAL
Hapa ni katika viwanja vya Butiama katika maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha mwalimu JULIUS KAMBARAGE NYERERE ambapo leo imetimia maiaka12 tangu kuaga dunia mwaka 1999 katika Hospitali ya St THOMAS huko LONDON UINGEREZA.

Sambamba na maadhimisho hayo makamu wa rais amewasha mwenge wa uhuru katika viwanja hivyo hivyo ambao umeanza kuzungushwa mkoani mara chini mkimbizaji mkuu wa mwaka huu.
Mwalimu nyerere akiwa miongoni mwa kuhutubia wananchi,itakumbukwa kwamba
Ni mmoja wa viongozi wachache wanaokumbukwa kwa kutojilimbikizia mali pamoja na kutawala kwa miaka zaidi ya 24.

Hapa ndipo mwili wake ulipohifadhiwa nyumbani kwake Butiama. 
Mwishoni mwa maisha yake Nyerere aliishi kama mkulima wa kawaida kijijini kwake Butiama. Alipatwa na kansa ya damu (leukemia) na kufariki Uingereza wakati wa kutibiwa katika mji wa London tarehe 14 Oktoba, 1999. Alizikwa mahali pa kuzaliwa kwake, kijiji cha Butiama.
                                                 Julius Kambarage Burito Nyerere 1960
     
Tarehe ya kuzaliwa
Mahali pa kuzaliwa
Tarehe ya kifo
Rais wa Tanzania
Alingia ofisini
1964
Aliondoka ofisini
1985
Alitanguliwa na
(alikuwa rais wa kwanza)
Alifuatwa na
Dini
Mkristo Mkatoliki
Elimu yake
Chuo Kikuu cha Edinburgh - Uskoti
Digrii anazoshika
M.A. ya historia na uchumi
Kazi
mwalimu, mwanasiasa
Mengine
Nyerere alikuwa mwenyekiti wa chama cha TANU na baadaye wa CCM.
Mara nyingi aliitwa "Mwalimu Nyerere".

Wednesday 12 October 2011

Itakumbukwa kuwa wiki iliyopita meli ya TAURANGA huko NEWZEELAND ikiwa na tani kadha za mafuta iligonga mwamba na mafuta kuanza kuvuja ambapo hadi sasa viumbe vimeshaanza kuathirika na mafuta hayo, lakini hii leo muda mfupi kutoka sasa imeonekana inaweza kuzama baada ya mafuta hayo kupungua upande na baadhi ya makontena kuanza kudondoka baharini.


Unavyoona katika picha hapa ni maili14 zikiwa ni kilomita 22 kutoka katika mji wa TAURANGA ambapo ilijaza kontena 70 lakini inasemekana aliyekuwa mwongozaji wa meli hiyo (CAPTAIN)ameshafunguliwa mashitaka na hiyo ni kwa mujibu wa msemaji STEVE JONES.
Ni meneja wa kampuni ya utalii ya KIROYERA Wlliam Rutta alipokuwa akichangia jinsi ya vyombo vya habari kuhamasisha ushiriki wa maadhimisho ya miaka hamsini ya uhuru mkoani kagera katika kikako cha mkuu wa mkoa wa kagera Fabian Inyas Masawe pamoja na wamiliki na waandishi wa habari.

Katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mkoa wa kagera Wiliam Ruta aliahidi kampuni yake kutoa kiasi cha shilingi laki8 kwa ajili ya mwandishi bora wa habari za uhuru ambapo mkuu wa mkoa ameongeza kiasi cha shiulingi laki mbili na kutimiza milioni moja kwa m,shindi huyo.

Hata hivyo kampun i ya KOROYERA itampeleka mwandishi huyo kupanda mlima kilimajaro ulipopandishwa mwenge wa uhuru mwaka 1961.

Monday 3 October 2011

SCANIA TANZANIA LTD in GYMKANA BUKOBA

Kumekuwa na tabia ya kufanya usafi pamoja na marekebisho ya baadhi ya miundombinu wakati wa ujio wa wageni mbalimba kitaifa na kimataifa.

Jambo ambalo limeonekana leo ni pale ambapo watu wanaosadikiwa kutoka halmashauri wameonekana wakizoa taka katika dampo ambalo lipo uchafu mwingi siku nyingi katika viwanja vya GYMKANA mjini bukoba kwasababu kuna uzinduzi wa maadhimisho.

Hii ni gari nambari STK 1113
Ni jambo la kushangaza na kusikitisha kuona watu wanaishi na uchafu siku zote wenyeji wanishi nao lakini wageni wakiingia hatua za haraka zinachukuliwa tuangalie picha hii ambayo imechukuliwa dakika chache kabla ya kuwasili mgeni rasmi jaji mkuu wa tanzania OTHMAN CHANDE katika viwanja hivyo.
                                         Ni katibu mkuu wa wizara ya afya na maendeleo ya jamii Bi BRANDINA NYONI akizungumza katika maadhimisho ya siku mbili ya afya katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam katika kipindi hiki cha miaka 50 ya uhuru.

Katika maadhimisho hayo yaliyoanza tarehe 30/09/2011na kuhitimishwa 2/10/2011wizara ya afya imewaambia wananchi kuwa makini kufuata ushauri mbalimbali ikiwa ni samamba na kutoa mawasiliano kwa wauguzi na kuahidi kuwa wizara hiyo iko tayari na inajali matatizo ya wagonjwa.

Katibu huyo amesema pamoja na mataifa ya afrika kuwa na tatizo la kuongezeka kwa vifo vya mama na mtoto wizara ya afya tanzania inajitahidi kupunguza  vifo hivyo nchini.

AKINA MAMA WALIOUZULIA MAADHIMISHO YA WIZARA YA AFYA.

MAONESHO YA WIKI YA USALAMA BARABARANI YAMEANZA KATIKA VIWANJA VYA GYMKANA MANISPAA YA BUKOBA 02/10/2011.
Kubwa nilililoshuhudia pale ni kwamba mabanda yamemuonesha na kuelezea mawili matatu lakini pamoja na hiyo vifaa mbalimbali vya usalama vimeoneshwa pamoja na vya kuzimia moto, maelezo ya matumizi sahihi ya barabara ni vitu vinayoelezwa sit u kwa mgeni rasmi bali wale wote wenye kutembelea maadhimisho hayo  wanafundishwa.
=kwanza tuwashukuru usalama barabarani mkoani kagera kama utakumbuka alhamisi tulifanya kipindi tukazungumzia mambo mengi kuhusu alama za barabarani kwakweli nimeona wamejitahidi japo ni kazi zao ila wameweka alama hizo.
=jambo linguine ambalo limejitokeza ni pale kwenye viwanja vya GYMKANA huwa kuna dampo la takataka, dampo hilo siku nyingi limejaa takataka lakini leo dakika chache kabla yta kuwasili mgeni rasmi niemona gari ambayo naweza kusema kuwa ni ya almashauri yenye nambari STK 1113 aina ya ISUZU INJECTION ikizoa uchafu.
=Jmbo lingine watanzania tunashindwa kuchangamkia fursa alafu tunalalamika kuwa hatujaambiwa kampuni ya skania imeskia uwepo wa maadhimisho ikaamua kufika katika maonesho na vifaa mbalimbali, nimezungumza na meneja wa scania Tanzania ltd badaye kidogo mtamskia.

Mgeni rasmi katika madhimisho haya jaji mkuu Tanzania OTHMAN CHANDE akisaini alipowasili katika banda kikosi cha usalama barabarani na chini anapewa maelezo kuhusu matumizi ya barabara. 


Balozi HAMIS SUED KAGASHEKI akiteta jambo JAJI MKUU alipowasili viwanja vya GYMKANA wakti wa maelezo madogo kutoka kwa kamanda wa polisi mkoa KAGERA.


Hapa jaji alikuwa akimsikiliza mtaalamu aliyeandaa alama za barabarni kuhusu walemavu lakini wakti huo naye ni mlemavu.

Ni alama za usalama barabarani kwa ajili ya walemavu zilizobuniwa na maalamu huyo.

Sunday 2 October 2011

Maazimisho ya kilele cha maadhimisho ya siku ya wazee duniani yaliyofanyika katika viwanja vya shirika la KWA WAZEE nshamba wilayani Muleba mkoani Kagera.

Katika maadhimisho hayo walizungumzia pensheni wakti wakilalamikia kuendelea kutozwa gharama za matibabu alhali serikali imeshasema kuwa watibiwe bure.

Jambo lingine la msingi katika maadhimisho hayo ambayo wazee wameona ni bora walitoe katika siku muafaka ni kupuuzwa na wahudumu wanapokuwa katika vituo vya huduma ya matibabu.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ya tarehe 01 oktoba 2011 alikuwa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya muleba, GEORGE KATOMERO.

Saturday 1 October 2011

Ni raia watu weusi nchini LIBYA jinsi wanavyotaabika katika viwanja mbalimbali nchini humo tangu kuanza machafuko ya kudai kung,olewa madarakani kwa KANAL MUHAMMAR GADAFFI.

SEHEMU YA NDANI YA UWANJA WA NDEGE WA SIRTE
Ijumaa Wanajeshi wanaoitii serikali ya mpito ya Libya wametwaa uwanja wa ndege katika mji wa Sirte, mahali alikozaliwa aliyekuwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi.
Wapiganaji walisonga mbele kupitia majengo ya uwanja wa ndege yaliyoharibiwa, wakiharibu miundombinu ambayo ilikuwa alama ya utawala wa Gaddafi.

Taarifa kuhusu alipo kiongozi huyo wa Libya, aliyeng'olewa madarakani, bado haijulikani lakini wengi wa wanafamilia wake wamekwisha kimbia kutoka Libya.
Wakaazi wengi wa manispaa ya Bukoba walimfahamu sana kijana huyu ambaye pamoja na kuwa na mapungufu ya akili, bado alijali sana usafi wake mwenyewe pamoja na kuvaa vizuri, lakini ni miezi kama miwili sasa tangu kugongwa na gari na kupoteza maisha katika barabara ya vibanda vya kuuzia kuku sokoni Bukoba.

Inasemekana aligongwa na gari ya kubeba mchnaga lakini dereva aliyegonga alikimbia na gari hilo na kushindwa kufahamika mara moja, jambo hilo bado lipo kwenye uchunguzi.

Lakini tunabaki na maswali kuwa inakuwaje watu wenye mapungufu wanagongwa na kupoteza maisha lakini matokeo au hatima ya wale walihusika na vifo hivyo hazifahamiki?

Ndani ya mwak huu aligongwa mtoto wa mitaani katika barabara ya uganda katika eneo la uswahili na aligongwa na miongoni mwa vijana wa mjini mfanyabiashara na baada ya kukamatwa aliwekewa dhamana jambo linaloruhusiwa kijamii lakini je hatima ni nini?
Ni rais mpya wa ZAMBIA MICHAEL SATTA  akitangaza baraza la mawaziri baada ya siku chache baada kushinda urais wa nchi hiyo.

Rais SATTA amemchagua pia makamu wake wa rais ambaye ni mzungu jambao ambalo limeleta mazungumzo na mafunzo kwa marais mbalimbali wa nchi za kiafrika na ulaya.

Katika uteuzi wake rais SATTA amefanya mchanganyiko kutoka vyama vya upinzani wake jambo ambalo linawezxa kuleta serikali yenye mwamko mzuri kisiasa.