MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday 14 October 2011

 Ujenzi holela unaoendelea kufanywa na wananchi wenye pesa zao katika manispaa ya Bukoba unasababisha maafa pamoja na kuharibu shughuli za maendeleo kwa baadhi ya watu na wakti mwingine kusasabisha maji kufunika madaraja ya mto kanoni ambayo hutumiwa na wananchi kupita kwa ajili ya shughuli zao za kila siku.

Pichani ni eneo linalopakana na hotel ya PRINCE mjini Bukoba ambpo kumefanyika ujenzi huo holela na kubadili mkondo wa mto kanoni ambo utokea kata za kagondo na nyanga ukikatiza katikati ya mji na kumwaga maji yake ziwa victoria.

Kutokana na ujenzi huu habari za uhakika kuhusu wanaotoa ruhusa ya watu hawa kujenga zinashindwa kudhibitishwa kwani wahusika wa halmashauri wanadai kuwa wananchi wanaamua kukaidi taratibu lakini kwa upande wa wajenzi wenyewe wanadai wamepewa hati za umiliki wa ardhi hvyo wana ruksa ya kujenga maeneo hayo.

Mvua zinapoanza kunyesha mkoani kagera manispaa inaathirika kwani baadhi ya makazi ya watu kama MUKIGUSHA maji uingia hadi ndani ya nyumba zao, kwingine biashara usimama kama inavyoonekana katika picha hapa chini.
Ni vibanda vya wafanyabiashara vimezingirwa na maji na shughuli zimesimama katika eneo la    PEDESTRIAN BRIDGE kanoni baada ya mvua iliyonyesha leo  Tarehe 14/10/2011.                  

No comments: