MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday 28 April 2015

WALIOPIMIWA VIWANJA MANISPAA YA BUKOBA, WASUBIRI CCM KUTATUA MZOZO

Ni wale wa viwanja 800 vilivyopimwa 2002, pamoja na vile 5000 vilivyopimwa 2011, malalamiko yanayokuja baada ya kutolipwa kiwango walichokuwa wakitakiwa kulipwa.
Ahadi hiyo ilikiukwa kwa kubadili kanuni kupitia sheria ya mipango miji ya mwaka 2007 (11)(2) kwa kutowasilisha rasimu rasimu ya mradi wa viwanja 5000 ili wajadili mpano huo ili wakubali au wakatae kama sheria inavyoelekeza.
Josephat Kyamwangire mzaliwa wa Bukoba mjini kata ya Kahoro, ni katibu wa walalamikaji waliotwaliwa viwanja elfu tano vilivyopimwa manispaa ya Bukoba, kinyume na makubaliano yao na viongozi wa halmashauri.

Katika upimaji huo wa viwanja wananchi wa manispaa Bukoba waliahidiwa kulipwa eneo linalochukuliwa na serikali, ilhaliwakisalia na kiwanja kimoja kama walivyoaidiwa na aliyekuwa meya wa manispaa hiyo Dr Anatory Aman.
Hatahivyo wananchi hawa wamenyimwa fursa yakumilikishwa viwanja katika maeneo yaoya awali baada ya manispaa kugawa viwanja vyote bila kuwapatia sehemu kama sera sheria na miongozo ya ardhi kupitia sera ya makazi 2000,kanuni ya ukadiriaji na ulipwaji wa fidia kupitia tangazo la serikali namba 78 na 79 la 2001.
Moja ya eneo lilopimwa na halmashauri katika manispaa ya Bukoba kwenye kata ya Nyanga.
Ripoti iliyotolewa na wizara ya adrhi mjini Dodoma 16 NOVEMBA, 2012,  Migogoro kati ya Jamii za Wakulima na Wafugaji, Migogoro kati ya Wanavijiji na Wawekezaji, Migororo ya Mipaka baina ya Mamlaka mbalimbali, Migogoro ya Wamiliki zaidi ya mmoja kwenye kiwanja kimoja, Uvamizi wa mashamba/viwanja, Migogoro ya Wananchi kutoridhika na fidia inayolipwa wakati wa utwaaji ardí.
Katika ya Wilaya 135 ni 86 to au asilimia 64% zilizo na Maafisa ardhi wateule. Hali hii inamaanisha kwamba Halmashauri nyingine hazina watendaji hawa kabisa au zinategemea walio katika Halmashauri jirani. Maafisa Ardhi 2 wamesimamishwa kazi. Wilaya ambazo zina watendaji chini ya asilimia hamsini ni Tabora, 33%, Mwanza Manispaa 43%; Katavi 33%; Lindi 33%.

Na Mwanaharakati.

KANDAYAZIWA KUREJEA KWA AINA MPYA.

 Ni wakati sasa wa kupata habari kwa njia ya mtandao www.kandayaziwaleo.blogspot.com kwa ukamilifu ambapo utaona video, utasikiliza sauti na kuona picha ilhali ukisoma kilichoandikwa kwa maelezo sahihi, kupitia KANDAYAZIWA BLOG.
 BOFYA HAPA KUSIKILIZA MOJA YA TAARIFA KUHUSU USHIRIKISHWAJI WAANDISHI HABARI NA MUSWADA WA SHERIA YA HABARI.

Kaa tayari kwa habari zaidi, COMING SOON.

Na Mwanaharakati.