MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday 20 December 2011

Ni chanzo cha maji ya mto KIGOYE katika kata ya Nshambya kwenye eneo la kyabitembe two.
 Haya ni baadhi ya majengo yakiwa katika bonde hili ndani ya chanzo cha maji kyabitembe Manispaa ya Bukoba.
 Majengo haya yapo ndani ya mita sitini kwenye chanzo cha maji, najiuliza viongozi wanaosisitiza kuwa sasa Bukoba itakuwa kama ulaya hawaoni wauzaji Holela wa viwanja?

Friday 9 December 2011

Mkuu wa mkoa (kushoto)aliongoza safu ya vingozi kufungua burdani ya muziki, nyuma yake ni Meya manispaa Anatoli Aman,katikati ni kamanda jeshi la polisi Enry Salewi, kulia Mkurugenzi manispaa Hamis Kaputa.
 Kanal masawe akiwalisha keki waliozaliwa tarehe 9 Desemba 1961.
 Keki ilikatwa kwa mbwembwe na mkuu wa mkoa.
 Kiongozi wa kidini KKKT.
 Askofu Mkuu msaidizi jimbo la Bukoba Methodius Kilaini.
 Shekh wa wilaya ya Bukoba Aruna Kichwabuta.
 Fabiani Masawe akikomelea katika hotuba kwa wananchi.
 Hii ndiyo Sura ya maadhimisho hayo.

Tuesday 29 November 2011

Maadhimisho miaka 50 ya uhuru mkoani kagera yapambwa na wanafunzi. Maonesho hayo yalianzia maandamano katika kata ya rwamishenye yakiongozwa na wanafunzi wenyewe ambapo kufikia kona ya kyakairabwa darajani walikutana na trafik (askari wa usalama barabarani) wakaanza kuwapanga ni jinsi gani wataingia uwanjani kyakairabwa.

Mgeni rasmi alikuwa mkuu wa mkoa wa kagera katika maadhimisho hayo lakini kwa hakika yalihudhuliwa na wanafunzi kwa wingi ambapo watu wazima wachache sana waliojitokeza walizungumza nami wakadai hawana maslahi na hawaoni cha kuwakusanya kutokana na kwamba serikali madarakani ndiyo inafaida ma maadhimisho si wananchi hivyo hakuna haja ya kuudhulia.

Meya wa manispaa ya Bukoba Bwana ANATOL AMAN alihijiwa nami moja kwamoja akakiri uchache wa wa raia hao lakini akatoa sababu kuwa wamekosekana kwasababu ni siku za kazi na kutokana na uchumi wananchoi wapo kwenye shughuli za utafutaji.

Wanafunzi wenyewe walisema wamelazimishwa na walimu na katika shule ya Buhembe Sec School waliandakwa majina ambaye hakufika atapewa adhabu.


Wednesday 23 November 2011

 Wanafunzi wa darasa la nne katika shule ya msingi ZAMZAM mjini BUKOBA wakivua samaki katika mto wenye maji machafu wa KANONI karibu kabisa na ofisi za Manispaa, muda wa saa tano asubuhi ambapo walitakiwa kuwa darasani.
 Ni jambo la kusikitisha kuona wazazi na walezi wakiwakuta watu hawa katika mazingira yanamna hiyo lakini hakuna anayekemea jambo hilo, je walimu hawajiulizi kwamba wanafunzi hawa wako wapi katika muda wa kuwa darasani?
 Huyu siyo kwamba amepumzika, ni mtu ambaye kafa baada ya kipigo kutoka kwa raia kwa mujibu wa vyanzo vyetu. Jamaa aliyefahamika kwa jina moja tu la NURU na inasemekana alikuwa akiishi katika vichaka vya NYAKANYASI mjini Bukoba, amekutwa amekufa karibu kabisa na daraja linalotenganisha mtaa wa nyakanyasi na USWAHILINI mjini Bukoba.
Miongoni mwa waliskia purkushani za usiku wakti wananchi wakitoa kichapo, wanasema waliskia sauti zikisema kama ndizi lakini hawakujua kulichoendelea.
Pembeni ni mizigo ya nguo inayosadikiwa kuwa ni ya wizi. Kumekuwa na matukio ya mauaji mjini bukoba ambapo m,apema mwezi uliopita mwanamke mmoja aliyefahmika kwa jina moja la NYANGOMA alikutwa amekufa katika mtaa wa BUYEKERA kata BAKOBA mjini BUKOBA wakti huo akiwa amevuliwa nguo yake ya ndani (chupi) na imetupwa pembeni

Friday 11 November 2011

ABIRIA WAKIRUDI KWENYE BASI BAADA YA KUCHIMBA DAWA MENEO YA CHATO.

Kuchimba dawa unapokuwa unasafiri katika basi kwa masafa marefu ni muhimu kwa ajili ya afya ya mwanadamu kwani safari zingine ni ndefu kutoka dar hadi bukoba au bukoba-dar, lakini ni kwamba uchimbaji huo wa dwa hauzingatii usafi wa mazingira.

Wanaposimamisha magari kwa ajili ya uchimbaji huo wa dawa pia umwaga uchafu wote unaokuwa ndani ya gari, si vibaya kufanya hivyo lakini jamani kumekuwa na kumwaga taka hizo maeneo yasiyofaa kama maeneo ya mitaro ya kusafisha maji ambayo inatakiwa kuwa safi muda wote
Ni mwezeshaji wa mfuko wa waandishi habari tanzania(TMF) Bwana JAPHET SANGA akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa DODOMA.

Amesisitiza waandishi kukamilisha kazi wanazoombea pesa kutoka TMF ili kuhimarisha uhaminifu katika mfuko huo ili utakapofunguliwa muhula mwingine mwaka 2012 waweze kupata ruzuku kwa urahisi.

TMF mwaka kesho 2012 inampango wa kurekebisha taratibu tofauti na za sasa ili kumwezesha mwandishi kupata ruzuku kwa haraka baada ya kuomba na wakti huo bwana SANGA akishauri kuwa kuanzia hapo TMF itakuwa na uataratibu wa kutomwonea mtu huruma ya kumpa pesa kama ataonekana kutokujali kazi yake ipasavyo.

Kuanzia mwishoni mwa novemba TMF itafunga muhula na kutoatoa ruzuku hadi mwezi march 2011.
NI WAANDISHI HABARI WAKIMSIKILIZA MWALIMU MWEZESHAJI(MENTOR) ALIYEVALIA KOFIA NA KOTI YA DRAFTI, MHARIRI  NDIMALA TEGAMBWAGE. 


BASI LINAPOSIMAMA AJILI YA KUCHIMBA DAWA.

Ni katika barabar ya Tabora Dar Wilayani IRAMBA katika maeneo ya MISIGIRI ambapo inaonekana kila mara gari hili pichani usimama hapa hili abiria wachimbe dawa lakini cha ajabu pamoja na uchimbaji huo wa dawa, wenye gari umwaga uchafu kama makopo ya soda na mifuko mbalimbali katika mtaro huu inavyooneka. Sasa je ukujaa mtaro huu itakuwaje?

Friday 4 November 2011

AFISA MAWASILIANO TACAIDS Bw RICHARD J. NGAIZA na MENEJA MAHUSIANO TACAIDS GRORY MZIRAY.

Waandishi habari wametakiwa kushirikisha jamii wanayoihudumia ili kushiriki mawazo na kujua matatizo yao kwa urahisi.

Hayo yamesemwa na meneja mahusiano wa TACAIDS Bi GRORY MZIRAY katika semina ya siku mbili kwa waandishi habari kanda ya ziwa kuhusu maandalizi ya vipindi vinavyohusu ugonjwa wa UKIMWI.

Amesema ugonjwa wa UKIMWI unaendelea kuwepo kwasababu ya wapenzi kuzoeana kwa muda mfupi, jambo linalopelekea kuacha kutumia kinga  baada ya kuwa pamoja katika mapenzi.

Naye Afisa mawasiliano TACAIDS Bwana RICHARD JOSEPH NGAIZA, amesema chombo cha habari cha ndani kinaifikia zaidi jamii ya eneo hilo kutokana na maelewano mazuri ya lugha inayotumika katika maeneo husika.

Semina hiyo ambayo inahitimishwa leo jijini Mwanza imeandaliwa na TACAIDS kwa ajili ya kuwajengea uwezo waandishi habari wa vyombo vya ndani (Community Radio) katika kanda ya ziwa ili kuwawezesha kuandaa vipindi kwa ufasaha na ujumbe uweze kufika kwa jamii kwa haraka zaidi.

Wednesday 19 October 2011

                                                            PORINI BUZIKU(CHATO)
Kumekuwa na taratibu za kukataza ukataji wa mkaa katika misitu ya hifadhi mkoani kagera lakini wakti huo mkoa huu ukiwa ni ule unaoongoza kuwa na gharama kubwa katika upatikanaji wa nishati mbadala.

Buziku ni moja ya misitu ya hifadhi ambayo imehifadhiwa kwa ajili ya mimea kitaifa lakini kwasasa ni sehmu ambayo imeshambuliwa na ukataji wa mkaa kwa kiasi kikubwa pamoja na uchungaji wa mifugo na kilimo katika msitu huo.

Kwenye picha huo ni baadhi ya magunia ya mkaa ambayo yameshuhudiwa na mtaalamu wa habari hizi wakti huo akiongea na wahusika wakasema kuwa wanafanya hivyo kwasababu ya maisha magumu.

Kwaupande wake afisa mali asli wa wilaya ya Chato bwana CHARLES SALEHE anasema msitu unapunguwa kwa kiasi kikubwa lakini wao kama wahusika wanakabiliwa na vitendea kazi ili kufanya doria za kutosha na baadhi ya wanasiasa wanahusika kuwadanganya wavamizi hao kwa kisingizio cha kuwapigia kura.
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM kata kagondo IGNATUS SIMON amekuta kondoo wake wanne wamechinjwa usiku wa kuamkia leo 19/10/2011 nyumbani kwake Kagondo karuguru katika manispaa ya Bukoba.

Akiongea na mwandishi habari hizi leo asubuhi mwenyekiti huyo amesema baada ya kuamka leo saa moja amekuta wamechinjwa pembezoni mwa zizi la kondoo hao wanne ambapo pia kilichomshangaza kutokuona damu zilizomwagika.

Akifafanua katika hilo amesema ametoa taarifa kituo cha polisi mjini Bukoba ambapo katika maelezo yake hakusita kueleza ugomvi alionao kwa jirani yake ambaye hakupenda kumtaja jina lakini akasema kuwa wamekuwa wakirumbana kwasababu za kisiasa na wakti huo pia wanagombea shamba ambapo kesi yao iko mahakamani.

Kondoo hao wamechinjwa usiku wa kuamkia leo siku ambayo walitarajia kumpeleka mwanasheria ili kukagua eneo linalogombewa hivyo alipofika naye ameshuudia hali hiyo.

Ripoti yake polisi ameitoa na kupewa RB NAMBA BU/RB/5619/2011.

Friday 14 October 2011

 Ujenzi holela unaoendelea kufanywa na wananchi wenye pesa zao katika manispaa ya Bukoba unasababisha maafa pamoja na kuharibu shughuli za maendeleo kwa baadhi ya watu na wakti mwingine kusasabisha maji kufunika madaraja ya mto kanoni ambayo hutumiwa na wananchi kupita kwa ajili ya shughuli zao za kila siku.

Pichani ni eneo linalopakana na hotel ya PRINCE mjini Bukoba ambpo kumefanyika ujenzi huo holela na kubadili mkondo wa mto kanoni ambo utokea kata za kagondo na nyanga ukikatiza katikati ya mji na kumwaga maji yake ziwa victoria.

Kutokana na ujenzi huu habari za uhakika kuhusu wanaotoa ruhusa ya watu hawa kujenga zinashindwa kudhibitishwa kwani wahusika wa halmashauri wanadai kuwa wananchi wanaamua kukaidi taratibu lakini kwa upande wa wajenzi wenyewe wanadai wamepewa hati za umiliki wa ardhi hvyo wana ruksa ya kujenga maeneo hayo.

Mvua zinapoanza kunyesha mkoani kagera manispaa inaathirika kwani baadhi ya makazi ya watu kama MUKIGUSHA maji uingia hadi ndani ya nyumba zao, kwingine biashara usimama kama inavyoonekana katika picha hapa chini.
Ni vibanda vya wafanyabiashara vimezingirwa na maji na shughuli zimesimama katika eneo la    PEDESTRIAN BRIDGE kanoni baada ya mvua iliyonyesha leo  Tarehe 14/10/2011.                  
MAKAMU WA RAIS MOHAMMED GHARIB BILAL
Hapa ni katika viwanja vya Butiama katika maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha mwalimu JULIUS KAMBARAGE NYERERE ambapo leo imetimia maiaka12 tangu kuaga dunia mwaka 1999 katika Hospitali ya St THOMAS huko LONDON UINGEREZA.

Sambamba na maadhimisho hayo makamu wa rais amewasha mwenge wa uhuru katika viwanja hivyo hivyo ambao umeanza kuzungushwa mkoani mara chini mkimbizaji mkuu wa mwaka huu.
Mwalimu nyerere akiwa miongoni mwa kuhutubia wananchi,itakumbukwa kwamba
Ni mmoja wa viongozi wachache wanaokumbukwa kwa kutojilimbikizia mali pamoja na kutawala kwa miaka zaidi ya 24.

Hapa ndipo mwili wake ulipohifadhiwa nyumbani kwake Butiama. 
Mwishoni mwa maisha yake Nyerere aliishi kama mkulima wa kawaida kijijini kwake Butiama. Alipatwa na kansa ya damu (leukemia) na kufariki Uingereza wakati wa kutibiwa katika mji wa London tarehe 14 Oktoba, 1999. Alizikwa mahali pa kuzaliwa kwake, kijiji cha Butiama.
                                                 Julius Kambarage Burito Nyerere 1960
     
Tarehe ya kuzaliwa
Mahali pa kuzaliwa
Tarehe ya kifo
Rais wa Tanzania
Alingia ofisini
1964
Aliondoka ofisini
1985
Alitanguliwa na
(alikuwa rais wa kwanza)
Alifuatwa na
Dini
Mkristo Mkatoliki
Elimu yake
Chuo Kikuu cha Edinburgh - Uskoti
Digrii anazoshika
M.A. ya historia na uchumi
Kazi
mwalimu, mwanasiasa
Mengine
Nyerere alikuwa mwenyekiti wa chama cha TANU na baadaye wa CCM.
Mara nyingi aliitwa "Mwalimu Nyerere".

Wednesday 12 October 2011

Itakumbukwa kuwa wiki iliyopita meli ya TAURANGA huko NEWZEELAND ikiwa na tani kadha za mafuta iligonga mwamba na mafuta kuanza kuvuja ambapo hadi sasa viumbe vimeshaanza kuathirika na mafuta hayo, lakini hii leo muda mfupi kutoka sasa imeonekana inaweza kuzama baada ya mafuta hayo kupungua upande na baadhi ya makontena kuanza kudondoka baharini.


Unavyoona katika picha hapa ni maili14 zikiwa ni kilomita 22 kutoka katika mji wa TAURANGA ambapo ilijaza kontena 70 lakini inasemekana aliyekuwa mwongozaji wa meli hiyo (CAPTAIN)ameshafunguliwa mashitaka na hiyo ni kwa mujibu wa msemaji STEVE JONES.
Ni meneja wa kampuni ya utalii ya KIROYERA Wlliam Rutta alipokuwa akichangia jinsi ya vyombo vya habari kuhamasisha ushiriki wa maadhimisho ya miaka hamsini ya uhuru mkoani kagera katika kikako cha mkuu wa mkoa wa kagera Fabian Inyas Masawe pamoja na wamiliki na waandishi wa habari.

Katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mkoa wa kagera Wiliam Ruta aliahidi kampuni yake kutoa kiasi cha shilingi laki8 kwa ajili ya mwandishi bora wa habari za uhuru ambapo mkuu wa mkoa ameongeza kiasi cha shiulingi laki mbili na kutimiza milioni moja kwa m,shindi huyo.

Hata hivyo kampun i ya KOROYERA itampeleka mwandishi huyo kupanda mlima kilimajaro ulipopandishwa mwenge wa uhuru mwaka 1961.

Monday 3 October 2011

SCANIA TANZANIA LTD in GYMKANA BUKOBA

Kumekuwa na tabia ya kufanya usafi pamoja na marekebisho ya baadhi ya miundombinu wakati wa ujio wa wageni mbalimba kitaifa na kimataifa.

Jambo ambalo limeonekana leo ni pale ambapo watu wanaosadikiwa kutoka halmashauri wameonekana wakizoa taka katika dampo ambalo lipo uchafu mwingi siku nyingi katika viwanja vya GYMKANA mjini bukoba kwasababu kuna uzinduzi wa maadhimisho.

Hii ni gari nambari STK 1113
Ni jambo la kushangaza na kusikitisha kuona watu wanaishi na uchafu siku zote wenyeji wanishi nao lakini wageni wakiingia hatua za haraka zinachukuliwa tuangalie picha hii ambayo imechukuliwa dakika chache kabla ya kuwasili mgeni rasmi jaji mkuu wa tanzania OTHMAN CHANDE katika viwanja hivyo.
                                         Ni katibu mkuu wa wizara ya afya na maendeleo ya jamii Bi BRANDINA NYONI akizungumza katika maadhimisho ya siku mbili ya afya katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam katika kipindi hiki cha miaka 50 ya uhuru.

Katika maadhimisho hayo yaliyoanza tarehe 30/09/2011na kuhitimishwa 2/10/2011wizara ya afya imewaambia wananchi kuwa makini kufuata ushauri mbalimbali ikiwa ni samamba na kutoa mawasiliano kwa wauguzi na kuahidi kuwa wizara hiyo iko tayari na inajali matatizo ya wagonjwa.

Katibu huyo amesema pamoja na mataifa ya afrika kuwa na tatizo la kuongezeka kwa vifo vya mama na mtoto wizara ya afya tanzania inajitahidi kupunguza  vifo hivyo nchini.

AKINA MAMA WALIOUZULIA MAADHIMISHO YA WIZARA YA AFYA.

MAONESHO YA WIKI YA USALAMA BARABARANI YAMEANZA KATIKA VIWANJA VYA GYMKANA MANISPAA YA BUKOBA 02/10/2011.
Kubwa nilililoshuhudia pale ni kwamba mabanda yamemuonesha na kuelezea mawili matatu lakini pamoja na hiyo vifaa mbalimbali vya usalama vimeoneshwa pamoja na vya kuzimia moto, maelezo ya matumizi sahihi ya barabara ni vitu vinayoelezwa sit u kwa mgeni rasmi bali wale wote wenye kutembelea maadhimisho hayo  wanafundishwa.
=kwanza tuwashukuru usalama barabarani mkoani kagera kama utakumbuka alhamisi tulifanya kipindi tukazungumzia mambo mengi kuhusu alama za barabarani kwakweli nimeona wamejitahidi japo ni kazi zao ila wameweka alama hizo.
=jambo linguine ambalo limejitokeza ni pale kwenye viwanja vya GYMKANA huwa kuna dampo la takataka, dampo hilo siku nyingi limejaa takataka lakini leo dakika chache kabla yta kuwasili mgeni rasmi niemona gari ambayo naweza kusema kuwa ni ya almashauri yenye nambari STK 1113 aina ya ISUZU INJECTION ikizoa uchafu.
=Jmbo lingine watanzania tunashindwa kuchangamkia fursa alafu tunalalamika kuwa hatujaambiwa kampuni ya skania imeskia uwepo wa maadhimisho ikaamua kufika katika maonesho na vifaa mbalimbali, nimezungumza na meneja wa scania Tanzania ltd badaye kidogo mtamskia.

Mgeni rasmi katika madhimisho haya jaji mkuu Tanzania OTHMAN CHANDE akisaini alipowasili katika banda kikosi cha usalama barabarani na chini anapewa maelezo kuhusu matumizi ya barabara. 


Balozi HAMIS SUED KAGASHEKI akiteta jambo JAJI MKUU alipowasili viwanja vya GYMKANA wakti wa maelezo madogo kutoka kwa kamanda wa polisi mkoa KAGERA.


Hapa jaji alikuwa akimsikiliza mtaalamu aliyeandaa alama za barabarni kuhusu walemavu lakini wakti huo naye ni mlemavu.

Ni alama za usalama barabarani kwa ajili ya walemavu zilizobuniwa na maalamu huyo.

Sunday 2 October 2011

Maazimisho ya kilele cha maadhimisho ya siku ya wazee duniani yaliyofanyika katika viwanja vya shirika la KWA WAZEE nshamba wilayani Muleba mkoani Kagera.

Katika maadhimisho hayo walizungumzia pensheni wakti wakilalamikia kuendelea kutozwa gharama za matibabu alhali serikali imeshasema kuwa watibiwe bure.

Jambo lingine la msingi katika maadhimisho hayo ambayo wazee wameona ni bora walitoe katika siku muafaka ni kupuuzwa na wahudumu wanapokuwa katika vituo vya huduma ya matibabu.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ya tarehe 01 oktoba 2011 alikuwa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya muleba, GEORGE KATOMERO.

Saturday 1 October 2011

Ni raia watu weusi nchini LIBYA jinsi wanavyotaabika katika viwanja mbalimbali nchini humo tangu kuanza machafuko ya kudai kung,olewa madarakani kwa KANAL MUHAMMAR GADAFFI.

SEHEMU YA NDANI YA UWANJA WA NDEGE WA SIRTE
Ijumaa Wanajeshi wanaoitii serikali ya mpito ya Libya wametwaa uwanja wa ndege katika mji wa Sirte, mahali alikozaliwa aliyekuwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi.
Wapiganaji walisonga mbele kupitia majengo ya uwanja wa ndege yaliyoharibiwa, wakiharibu miundombinu ambayo ilikuwa alama ya utawala wa Gaddafi.

Taarifa kuhusu alipo kiongozi huyo wa Libya, aliyeng'olewa madarakani, bado haijulikani lakini wengi wa wanafamilia wake wamekwisha kimbia kutoka Libya.
Wakaazi wengi wa manispaa ya Bukoba walimfahamu sana kijana huyu ambaye pamoja na kuwa na mapungufu ya akili, bado alijali sana usafi wake mwenyewe pamoja na kuvaa vizuri, lakini ni miezi kama miwili sasa tangu kugongwa na gari na kupoteza maisha katika barabara ya vibanda vya kuuzia kuku sokoni Bukoba.

Inasemekana aligongwa na gari ya kubeba mchnaga lakini dereva aliyegonga alikimbia na gari hilo na kushindwa kufahamika mara moja, jambo hilo bado lipo kwenye uchunguzi.

Lakini tunabaki na maswali kuwa inakuwaje watu wenye mapungufu wanagongwa na kupoteza maisha lakini matokeo au hatima ya wale walihusika na vifo hivyo hazifahamiki?

Ndani ya mwak huu aligongwa mtoto wa mitaani katika barabara ya uganda katika eneo la uswahili na aligongwa na miongoni mwa vijana wa mjini mfanyabiashara na baada ya kukamatwa aliwekewa dhamana jambo linaloruhusiwa kijamii lakini je hatima ni nini?
Ni rais mpya wa ZAMBIA MICHAEL SATTA  akitangaza baraza la mawaziri baada ya siku chache baada kushinda urais wa nchi hiyo.

Rais SATTA amemchagua pia makamu wake wa rais ambaye ni mzungu jambao ambalo limeleta mazungumzo na mafunzo kwa marais mbalimbali wa nchi za kiafrika na ulaya.

Katika uteuzi wake rais SATTA amefanya mchanganyiko kutoka vyama vya upinzani wake jambo ambalo linawezxa kuleta serikali yenye mwamko mzuri kisiasa.