MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday 30 June 2017

AUDIO; MARUFUKU KUZUIA WANANCHI KUJIANDIKISHA NIDA KWASABABU ZA VITAMBULISHO



Afisa msajili wa vitambulisho vya taifa NIDA, ambaye sasa yupo mkoani Kagera kusimamia uandikishaji katika manispaa ya Bukoba Bi. Sophia Mfinanga,  amesema kuwa hakuna ulazima wa vitambulisho hivyo, kwasababu kinachoendelea sasa ni utambuzi na uandikishaji wa wananchi katika daftari la kudumu la makazi.

Ameagiza watendaji wa kata, mitaa kutokuwazuia wananchi wanaojitokeza kuandikishwa, na mwananchi hatakiwi kuondoka na fomu hiyo, badala yake ijaziwe hapohapo kwenye ofisi za kata au mtaa chini ya uangalizi wa mtendaji au mwenyekiti.

Amesema kuwa mamlaka ya vitambulisho vya taifa NIDA, tarehe 30/05/2017 ilitoa elimu yaani mafunzo elekezi kwa wenyeviti wa mitaa na ilitoa mafunzo kwa watendaji mitaa na kata ikiwa ni tarehe 9/06/2017,  hivyo uandikishaji utaendelea hadi 15/07/2017, na hakuna kuwazuia kuandika kwa kukosa cheti cha kuzaliwa, viapo pamoja na vitambulisho vingine kama leseni, kadi ya mpiga kura au vyeti vya shule, kwani kama kutakuwa na lazima hiyo wataelekezwa na maofisa wa uhamiaji.
Siku chache zilizopita, Mtendaji wa kata ya Bakoba katika manispaa ya Bukoba na wengine watatu, wameshikiliwa na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU mkoani Kagera, kwa kuwatoza wananchi shilingi elfu tano katika uandikishaji wa vitambulisho vya taifa.
Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu, mkuu wa Takukuru mkoani Kagera Joseph Mwaiswelo, alisema kuwa  pamoja na kukamatwa kwa mtendaji huyo, pia inawashikiria watu watatu na wanaendelea kuhojiwa.

Alimtaja mtendaji huyo kuwa Marco Mgoe, huku akisisitiza kuwa majina ya wengine yanahifadhiwa kwa sababu za uchunguzi, na kuwa wanatuhumiwa kwa kutoza wananchi shilingi elfu tano kwa ajili ya kupewa fomu za vitambulisho vya taifa wakati wa uandikishaji unaoendelea. 

Na Mwanaharakati.

Thursday 29 June 2017

VIDEO;KITU CHA TOFAUTI KATIKA MAONYESHO YA SABASABA MSIMU HUU




July 4 mwaka huu umefanyika uzinduzi rasmi wa maonyesho ya sabasaba mkoani Kagera ambapo mkuu wa wilaya Bukoba Deodatus Kinawilo alifanya uzinduzi huo kwa niaba ya mkuu wa mkoa Kagera. 

Akizindua maonyesho hayo ambayo yatafikia kilele july 9 mwaka huu,amewashauri baadhi ya washiriki wa maonyesho hayo kushirikiana kwa karibu na halmashauli kwa kuwashirikisha kile wanachokifanya ili kuhakikisha Tanzania ya viwanda inafanikiwa kwa asilimia kubwa.

Aidha amesema kuwa serikali inatambua changamoto wanazokumbana nazo katika kuendesha biashara yao,ambapo ni pamoja na maeneo ya kufanyia biashara sambamba na mitaji midogo,na kuahidi kuwa serikali inaangalia na kwa jinsi gani itawasaidia juu ya changamoto hizo.

Sanjali na hayo Mh.Kinawilo amesema kuwa muda wowote ndani ya mwezi huu serikali itazindua mpango wa kuendeleza sekita ya kilimo awamu ya pili ambapo mpango huo unalenga kufanya m apinduzi  ili wakulima walime kutoka kilimo cha kujikimu na kwenda kwenye kilimo cha biashara.

TAZAMA VIDEO YA DC BUKOBA

Na Mwanaharakati.

Wednesday 28 June 2017

KAULI YA DC KINAWIRO JUU YA ZAO LA CHAI



Uzalishaji wa chai katika kiwanda cha Kagera tea limited, umeshuka kutoka kilo elfu 60 za chai kwa siku hadi kilo kati ya elfu 30 hadi 45 kwa wiki moja.
Kushuka huko kumetokana na wakulima kupunguza au kukata tamaa ya kulima zao hilo .

Akitoa taarifa kwa mkuu wa wilaya ya Bukoba,  mkurugenzi mtendaji wa kiwanda hicho Dokta Peter Mgimba, amesema kuwa wakulima wametelekeza mashamba ya zao hilo, kutokana na bei kutopandishwa ikilinganishwa na mazao mengine.
Baada ya kusikiliza matatizo ya kiwanda hicho, mkuu wa wilaya ya Bukoba Bw. Deodartus Kinawiro,  ametoa agizo kwa uongozi wa halmashauri ya wilaya Bukoba, kubuni mbinu mbadala za  kufufua zao la chai kwa wananchi wake, kwa kuwaletea maendeleo na kuokoa kufifia kwa zao hilo.

Kiwanda cha chai cha kagera tea limited kimetakiwa kulipa deni la zaidi ya shilingi milioni 30 wanazodaiwa na gereza la Rwamurumba  ifikapo julai mwaka huu kama ilivyoelekezwa na mahakama.


Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa wilaya Bukoba Deodatus Kinawiro mara baada ya kupokea  taarifa kutoka kwa kaimu Mkuu wa gereza la Rwamurumba ASP Focus Kagoroba  ambaye amesema kuwa anashangazwa na uongozi wa kiwanda hicho kushindwa kulipa deni hilo wakati Mahakama imekwishaweka taratibu za ulipaji deni hilo. 

Bwana Kinawiro amesema kuwa ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza ikiwemo ya utafishaji wa baadhi ya mali za kiwanda ,uongozi wa kiwanda hicho unatakiwa kulipa  deni hilo haraka iwezekanavyo.

Mkurugenzi wa kiwanda hicho amekili uwepo wa deni hilo ambapo amesema kuwa atahakikisha analipa fedha hizo kwa wakati kama ilivyoagizwa.

Aidha ameongeza kuwa kwa sasa kiwanda hicho kinadaiwa kiasi cha shilingi milioni tatu  malipo ya wakulima kwa kipindi cha mwezi mei na amesema kuwa mchakato wa ulipaji wa madeni hayo utafanyika hivi karibuni ili kunufaisha wakulima wa zao hilo.
 

Mkuu huyo wa wilaya ametumia nafasi hiyo  kuwataka viongozi wa chama cha wakulima wa chai mkoani Kagera, kuacha kuwa wanaharakati ,bali wafanye kazi yao kwa malengo ya kujiletea maendeleo.

Na Mwanaharakati.

AUDIO; TAKUKURU YASHIKILIA WANNE KWA KUTOZA PESA UANDIKISHAJI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA KAGERA



Mtendaji wa kata ya Bakoba katika manispaa ya Bukoba na wengine watatu, wanashikiliwa na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU mkoani Kagera, kwa kuwatoza wananchi shilingi elfu tano katika uandikishaji wa vitambulisho vya taifa.

Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu, mkuu wa Takukuru mkoani Kagera Joseph Mwaiswelo, amesema kuwa  pamoja na kukamatwa kwa mtendaji huyo, pia inawashikiria watu watatu na wanaendelea kuhojiwa.


Amemtaja mtendaji huyo kuwa Marco Mgoe, huku akisisitiza kuwa majina ya wengine yanahifadhiwa kwa sababu za uchunguzi, na kuwa wanatuhumiwa kwa kutoza wananchi shilingi elfu tano kwa ajili ya kupewa fomu za vitambulisho vya taifa wakati wa uandikishaji unaoendelea.

Amesema kuwa katika uandikishaji huo, fomu zinatolewa bure na serikali, hivyo wananchi wasidanganyike kutozwa pesa bila ufafanuzi wa kazi yake.
Mwaiswelo amesema kuwa wanaendelea na kuwahoji watuhumiwa, na ikiwa upelelezi utakamilika watu hao watafikishwa mahakamani.
 

Na Mwanaharakati.