MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday 28 June 2017

KAULI YA DC KINAWIRO JUU YA ZAO LA CHAI



Uzalishaji wa chai katika kiwanda cha Kagera tea limited, umeshuka kutoka kilo elfu 60 za chai kwa siku hadi kilo kati ya elfu 30 hadi 45 kwa wiki moja.
Kushuka huko kumetokana na wakulima kupunguza au kukata tamaa ya kulima zao hilo .

Akitoa taarifa kwa mkuu wa wilaya ya Bukoba,  mkurugenzi mtendaji wa kiwanda hicho Dokta Peter Mgimba, amesema kuwa wakulima wametelekeza mashamba ya zao hilo, kutokana na bei kutopandishwa ikilinganishwa na mazao mengine.
Baada ya kusikiliza matatizo ya kiwanda hicho, mkuu wa wilaya ya Bukoba Bw. Deodartus Kinawiro,  ametoa agizo kwa uongozi wa halmashauri ya wilaya Bukoba, kubuni mbinu mbadala za  kufufua zao la chai kwa wananchi wake, kwa kuwaletea maendeleo na kuokoa kufifia kwa zao hilo.

Kiwanda cha chai cha kagera tea limited kimetakiwa kulipa deni la zaidi ya shilingi milioni 30 wanazodaiwa na gereza la Rwamurumba  ifikapo julai mwaka huu kama ilivyoelekezwa na mahakama.


Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa wilaya Bukoba Deodatus Kinawiro mara baada ya kupokea  taarifa kutoka kwa kaimu Mkuu wa gereza la Rwamurumba ASP Focus Kagoroba  ambaye amesema kuwa anashangazwa na uongozi wa kiwanda hicho kushindwa kulipa deni hilo wakati Mahakama imekwishaweka taratibu za ulipaji deni hilo. 

Bwana Kinawiro amesema kuwa ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza ikiwemo ya utafishaji wa baadhi ya mali za kiwanda ,uongozi wa kiwanda hicho unatakiwa kulipa  deni hilo haraka iwezekanavyo.

Mkurugenzi wa kiwanda hicho amekili uwepo wa deni hilo ambapo amesema kuwa atahakikisha analipa fedha hizo kwa wakati kama ilivyoagizwa.

Aidha ameongeza kuwa kwa sasa kiwanda hicho kinadaiwa kiasi cha shilingi milioni tatu  malipo ya wakulima kwa kipindi cha mwezi mei na amesema kuwa mchakato wa ulipaji wa madeni hayo utafanyika hivi karibuni ili kunufaisha wakulima wa zao hilo.
 

Mkuu huyo wa wilaya ametumia nafasi hiyo  kuwataka viongozi wa chama cha wakulima wa chai mkoani Kagera, kuacha kuwa wanaharakati ,bali wafanye kazi yao kwa malengo ya kujiletea maendeleo.

Na Mwanaharakati.

No comments: