MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 28 August 2014

HAYAWI HAYAWI!!! FAINALI YA TMT JUMAMOSI HII.

Na Mwanaharakati.

DC BUKOBA AKABIDHI BAISKELI KWA WAJASRIAMALI WANANWAKE MANISPAA YA BUKOBA.

 Kikundi cha Wanawake Wajasiriamali, kinachojihusisha na Usindikaji wa vyakula manispaa ya Bukoba kimepatiwa wa Baiskeli 39 ili ziweze kuwasaidia Wajasiriamali hao katika shughuli zao za uzalishaji.


                                     
 Picha juu ni Bi Ziporah Pangani, mkuu wa wilaya Bukoba, akipewa maelezo na mratibu wa kikundi Bi Jesca Jonathan, alipowasili kwenye ofisi yao.
 
 Akikabidhi Baiskeli hizo, mkuu wa wilaya ya Bukoba , ZIPORAH PANGANI amewahimiza wanawake hao kuendelea na umoja huo,  kwani kupitia kikundi hicho wameweza kufanya shughuli zao za kimaendeleo.


Akisoma risala ya wana kikundi,  Mratibu wa kikundi hicho JESKA JONATHAN amesema kuwa, kikundi kina jumla ya wanachama 425 ambao wamekuwa wakijihusisha na shughuli za kilimo na usindikaji vyakula.

Na Mwanaharakati.

Wednesday 27 August 2014

NEWS ALERT!!! RAIS KIKWETE WA TANZANIA, AMPONGEZA RAIS WA BURUNDI PIERRE NKURUNZIZA, BAADA KUHAKIKI MIPAKA YA NCHI HIZO MBILI

Moja ya alama ya mpaka unaotenganisha Tanzania na Burundi ikiwa imekamilika katika eneo la Mugikomero, wilayani Ngara kama  mipaka ya kimataifa.
Raia wa Burundi wakiwa nyuma ya alama ya mpaka  inayotenganisha Tanzania na Burundi.

Na Mwanaharakati.

TANZANIA; JWTZ YASHINDA MPIRA WA KIKAPU KWA WANAWAKE



Praiveti Mwanaidi Hassan akiifungia timu ya JWTZ goli la 36 dhidi ya 30 ya Uganda na kuibuka mshindi wa kwanza Netball kwa mara ya nane mfululizo kwenye michezo ya majeshi ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, Zanzibar .
 

Na Mwanaharakati.

HATARI YA VIFO VIWANDANI YAENDELEA MKOANI PWANI.

Siku chache baada ya mtanzania kugundulika amesagwa na machine na taarifa zake kutoripotiwa katika kiwanda kimoja, huku mwingine akilipukiwa na mtungi wa gesi usoni katika kinu cha kuyeyusha chuma chakavu katika kiwanda kingine, mchina mmoja naye asagwa na machine na kubaki vipandevipande.

Taarifa inasmea kuwa mchina huyo ni wa kiwanda cha SUNSHINE LTD, kilichopo mjini Kibaha Pwani, amesagwa na moja ya mashine za kiwanda hicho ambapo inasemekana mchini mwenzake aliwasha mashine hiyo bila kujua kama mwenzake yuko ndani yake kwa shughuli za kitaalamu, na wakaja gungua mashine imeshaanza kumsaga, ambapo jitiada za kumwokoa zilifanikiwa kukusanya vipande vya mwili wake tu.

Kiwanda hicho kinajishughulisha na uzalishaji wa GYPSUM, ambapo wakati jicho letu linafika pale juzi, lilikuta jitihada za kuchoma vipande vya mwili wa mchina huyo zikifanywa, huku wenzie wakijitahidi kuficha taarifa zake.

Jitiada za kuendelea kupata taarifa za viwanda na utendaji wake zinaendelea ili tukujuze yanayotendekea na kwanini, lakini je wahusika na wafanyaje katika hayo na hasa wizara ya kazi na ajira pamoja na ya viwanda na biashara.
Na Mwanaharakati.

NEWS ALERT!!! MAUAJI KWA IMANI ZA KISHIRIKINA VYATOKEA GEITA

WATU wawili wameuawa kwa  kukatwakatwa   mapanga na watu wasiojulikana kwa imani za kishirikina  katika mkoa wa Geita.

Tukio hilo limetokea tarehe 20  mwezi huu majira ya  saa mbili usiku katika kijiji cha Hililika kata  ya Bukoli wilayani Geita, Mkoani hapa.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoani hapa Peter Kakamba alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja waliouwawa kuwa ni Agines Mihayo (22) na Nyanjige Mtula(65) wote wasukuma na wakazi wa kijijij hicho.

Kamanda Pita aliongeza kuwa Agnes ni jirani yake na Nyanjige na siku hiyo Agnes alikwenda kwa Nyanjige kumtembelea kama jirani yake na alipofika alikuta anakula naye alianza kula kabla hawajamaliza inasadikika watu wasiofahamika walikuja na kuanza kuwakata mapanga na kuwauwa palepale na kutokomea kusikojulikana.

Uchunguzi wa Tukio hilo unaendelea ili kubaini chanzo cha tukio hilo na watuhumiwa wa tukio hilo wanatafutwa na jeshi la polisi  kwa ajili ya kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Matukio ya kuwauwa vikongwe kwa imani za kishirikina katika Mkoa wa Geita yanazidi kushamiri huku wananchi wakiomba serikali kuwapa  kanda mahalum kama mkoa wa mara huenda matukio ya mauaji yanaweza kupungua.

Na Mwanaharakati.

MUHIMU SANA!!!UGONJWA WA KIFUA KIKUU NA UKOMA SASA KUKABILIWA


Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashidi akiwasha moja ya kati ya magari manne. 
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashidi (kulia) akipokea ufunguo wa moja ya gari kutoka kwa mwakilishi wa shirika la GLRA nchini Burchard Rwamtoga (kushoto)

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashidi (kulia) akimkabidhi Mratibu wa huduma za kifua kikuu na ukoma mkoa wa Kigoma Dkt. Deus Leonard (kushoto) moja kati ya magari manne  yaliyokabidhiwa kwa Serikali.


Mikoa ambayo imenufaika na msaada huo ni pamoja na Tanga, Kigoma, na Mikoa ya Kanda Maalum ya Ilala na Kinondoni.

Akipokea msaada huo leo (Jumanne Agosti 26, 2014) Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashidi (Mb) aliwataka Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kusimamia kikamilifu matumizi ya vyombo hivyo vya usafiri kwa kuvilinda na kuvitumia kulingana na malengo yaliyokusudiwa. 

Dkt. Seif alisema kuwa vifaa hivyo vimegawiwa kulingana na mgawanyo wa mikoa iliyoanishwa na Serikali katika Mpango wa Taifa wa kudhibiti ugonjwa wa kifua kikuu na ukoma.

Dkt. Seif alisema Mpango wa Taifa wa kudhibiti kifua kikuu na ukoma umekuwa na mafanikio ambapo  imeendelea kutoa matibabu kwa wagonjwa wote wa kifua kikuu na ukoma bila malipo katika hospitali na vituo vya huduma za afya vya serikali na binafsi nchini.

Aidha, Dkt. Seif amesema kuwa Tanzania imevuka malengo ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa kuponyesha asilimia 85 ya wagonjwa wote wa kifua kikuu wanaoanza matibabu kila mwaka.

“Takwimu zinaonesha kuwa Tanzania imefikia viwango vya asilimia 88 ya kuwahudumia na kuwaponyesha wagonjwa hao ambayo ni zaidi ya kiwango cha WHO” alisema Dkt Seif.

Dkt. Seif amesema kuwa kwa upande wa ugonjwa wa ukoma, Serikali inaendelea kufanya kampeni katika mikoa ya Dar es salaam, Dodoma, Kagera, Lindi, Morogoro, Mwanza, Pwani, Rukwa, Shinyanga, Tabora na Tanga katika kutoa elimu kwa wananchi namna ya kujikinga na ugonjwa huo.

Kwa mujibu wa Dkt. Seif alisema wagonjwa wapya wa ukoma waliogunduliwa mpaka sasa na kupatiwa tiba ni 23,667, na Serikali tayari imetoa jozi 35,000 ya viatu maalumu  kwa wagonjwa hao.

“Mpaka sasa tumeweza kufikia malengo ya kimataifa ya kutokomeza ukoma kwa kuwa chini ya mgonjwa mmoja katika watu 10,000 na kufanya ugonjwa wa ukoma kuwa si tatizo kubwa la kiafya kwa jamii nchini” alisema Dkt Rashid.

Naye mwakilishi wa shirika lisilo la kiserikali la GLRA nchini Burchard Rwamtoga  aliusifu kwa ushirikiano uliodumu kwa miaka 37 baina ya Shirika hilo na Serikali ya Tanzania katika mapambano ya magonjwa ya ukoma na kifua kikuu.

Aidha, Rwamtoga aliongeza kuwa Shirika la GLRA hutoa wastani wa Tsh. Bilioni 1.3 kila mwaka kwa Serikali  na kati ya fedha hizo kiasi cha Tsh.milioni 600 hutumika kwa ajili ya manunuzi ya vifaa vya usafirishaji ikiwemo magari, na pikipiki kwa waratibu wa kifua kikuu na ukoma. 

GLRA mbali na kutoa fedha kwa Serikali pia tunaratibu mpango wa  kuwajengea uwezo wa kiutendaji waratibu wa mikoa ikiwemo kutoa mafunzo nje ya nchi kupitia kituo cha ALERT kilichopo nchini Ethiopia, ambacho hujisihusha na mafunzo ya upasuaji na kutoa visaidizi ikiwamo miguu bandia na baiskeli kwa wagonjwa.

Kwa upande wake Mratibu wa huduma za kifua kikuu na ukoma mkoa wa Ilala Dkt. Mbarouk Seif ameishukuru Serikali kuupatia mkoa huowake gari la wagonjwa na kuahidi kuwa Ofisi yake itahakikisha gari hilo linawafikia na kuwahudumia wagonjwa kwa wakati.

Shirika la GLRA ilianza kusaidia wagonjwa wa ukoma nchini mwaka 1959 na kupata usajili mwaka 1977 ambapo lilianza kushirikiana na Mpango wa Kudhibiti kifua kikuu na ukoma (NTLP) nchini uliopo chini ya Wizara ya Afya na Usatawi wa Jamii.
 

Na Mwanaharakati.