MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday 27 August 2014

NEWS ALERT!!! MAUAJI KWA IMANI ZA KISHIRIKINA VYATOKEA GEITA

WATU wawili wameuawa kwa  kukatwakatwa   mapanga na watu wasiojulikana kwa imani za kishirikina  katika mkoa wa Geita.

Tukio hilo limetokea tarehe 20  mwezi huu majira ya  saa mbili usiku katika kijiji cha Hililika kata  ya Bukoli wilayani Geita, Mkoani hapa.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoani hapa Peter Kakamba alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja waliouwawa kuwa ni Agines Mihayo (22) na Nyanjige Mtula(65) wote wasukuma na wakazi wa kijijij hicho.

Kamanda Pita aliongeza kuwa Agnes ni jirani yake na Nyanjige na siku hiyo Agnes alikwenda kwa Nyanjige kumtembelea kama jirani yake na alipofika alikuta anakula naye alianza kula kabla hawajamaliza inasadikika watu wasiofahamika walikuja na kuanza kuwakata mapanga na kuwauwa palepale na kutokomea kusikojulikana.

Uchunguzi wa Tukio hilo unaendelea ili kubaini chanzo cha tukio hilo na watuhumiwa wa tukio hilo wanatafutwa na jeshi la polisi  kwa ajili ya kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Matukio ya kuwauwa vikongwe kwa imani za kishirikina katika Mkoa wa Geita yanazidi kushamiri huku wananchi wakiomba serikali kuwapa  kanda mahalum kama mkoa wa mara huenda matukio ya mauaji yanaweza kupungua.

Na Mwanaharakati.

No comments: