MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday 28 February 2014

RUSHWA MANISPAA BUKOBA; TAKUKURU YAKUTANA NA WAZEE

TAKUKURU yaitaka jamii imetakiwa kuelewa kuwa kuporomoka kwa maadili kunasababisha uwepo wa rushwa nchini.
AFISA MKUU TAKUKURU MKOANI KAGERA AKIZUNGUMZA NAMI
 
Mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU, Bwana JOSEPH MWAISWELO, katika semina maalumu ya maadili kwa wazee wa manispaa ya Bukoba, katika mpango wa taasisi hiyo nchi nzima kuhakikisha waelimisha kuhusu maadili ambapo mwaka huu wameanza na wazee.
Amesema kuwa pamoja na maadili, umasikini pia unasababisha kuongezeka kwa rushwa hivyo TAKUKURU imetambua hayo na kuamua kuanza na wazee ambapo pia wanashughulika na wanafunzi wa shule za msingi
Bwana Mwaiswelo amesema kuwa rushwa nchini inaongezeka, hivyo jamii itambue kuwa ni lazima maadili yazingatiwe, huku baadhi ya wazee waliopewa semina hiyo na kutoa michango yao, ni pamoja na shekh wa mkoa ARUN KICHWABUTA,(hayupo pichani) aliyesisitiza kuwa malezi bora ndiyo njia pekee ya kusaidia kizazi cha sasa, ambapo amewata wazazi na walezi, kuwapa ushirikiano wa kutosha walimu kuhusu watoto wao.

Katibu wa CCM manispaa ya Bi JANET KAYANDA,(hayupo pichani) kwa upande wake amesema kuwa jambo la maadili siyo nla sekta Fulani, bali serikali madarakani, wanasiasa na wataalamu pamoja na mwananchi mmoja mmoja wanatakiwa kushirikiana pamoja, kwani akili inaendana na maadili.

 Pichani ni ANNET MWAKATOBE, mkuu wa dawati la elimu TAKUKURU mkoani Kagera.
MWANA HARAKATI

WAETHIOPIA WAKAMATWA KAGERA

Ni wahamiaji haramu 5 kutoka Somalia ambao kwa taarifa kutoka ofisi ya uhamiaji mkoani Kagera wameingilia mpakani Mtukula.
 Kwa mjibu wa ofisa kutoka uhamiaji JEREMIAH MWAKIBINGA aliyezungumza kwa niaba wa kamishna msaidizi George Kombe, amewasisitiza wananchi kuacha kujihusisha na kukaribisha wahamiaji hao.

Amesema kuwa uhamiaji Kagera, leo imekamata wahamiaji5 ambao wa Passpot zao lakini hakufuata sheria za kuingia nchini, huku akisema kuwa wiki iliyopita walikamata wahamiaji haramu 3 kutoka Somalia, na taratibu za kisheria zikafuata mkondo wake.

Amewataja wa Ethioppia hao kuwa ni BAHR KECHINE, ACHEMU LAPHISO, GIZACHEW SHAIMELO, ZEKERYE EDASA ABATE na ZELEKE ASSEFA,  wote wanaume vijana.

MWANA HARAKATI

BREACKING NEWS!!! WANNE WAFA PAPO HAPO AJALI YA BASI NA TREN

Taarifa za awali zinasema ni bas la Bunda ambalo limegongwa kwenye kivuko cha treni mkoani Singida.

                                                        Wananchi wakishuudia baada ya ajali
                                         Juu ni Tren iliyosababisha ajali na chini hali ya basi lenyewe.
Mpaka sasa ni watu 4 wamethibitika kufa na tunaendelea kufuatilia habari zaidi juu ya tukio hilo ikiwemo sababu ya msingi ya kusababisha ajali hiyo.

Tutaendelea kuwajuza zaidi chochote kitakachojiri kwa undani.

MWANA HARAKATI