MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday 31 July 2015

MAZITO YAIBUKA KAMPEIN KURA YA MAONI MANISPAA BUKOBA.



. Baadhi ya wajumbe wazomewa,
. Waliokosa majibu ya wananchi watimuliwa,
. Upigaji kura jumamosi tarehe 1.

Ni katika mikutano 12 ya kampeini za kuomba kura kwa watia nia ya ubunge manispaa ya Bukoba, ambapo wamezunguka kwa pamoja kata 14 za manispaa hiyo, huku baadhi ya wagombea wakizomewa, na wengine kuulizwa maswali kuhusu walichofanya awali na wengine kuhusu dhuluma walizosimamia huku majibu yakikosekana.
Jumla ya watia nia hao ni 8 ambapo kila mgombea amekumbana na maswali, kuzomewa au kushnagiliwa, kulingana na anavyofahamika katika kazi yake, na aliyeongoza kuzomewa na kukimbia mikutano alikuwa Anatory Aman, huku Mjuni Kataraiya akizomewa baada ya kujibu swali kuwa anglau alitoa lift, baada ya kuulizwa anachoweza kukumbukwa wakati akiwa mbunge.
George Lubaiyuka amejieleza kuwa amekuwa akifanya kazi za elimu kwa muda mrefu na sasa ni afisa elimu wilayani Misenyi, ameulizwa swali na kijana wa kata Ashai jinsi anavyoweza kusaidia kuondoa mkanganyiko katika ngazi ya ubunge ilhali kwenye sekta ya ualimu imekuwa ngumu huku walimu wakibainika kulalamika na yeye akiwa afisa elimu.


Anatory Amani aliwahi kuwa Meya na amesema kuwa yuko tayari kuwaletea maendeleo, lakini ameulizwa
swali na mmoja wa wajumbe kuwa ameongoza kuwa na kesi nyingi mahakamani huku akikataa maridhiano kama inavyoshauriwa kwenye chama chao, akipata nafasi ya ubunge hataongeza migogoro na hata kufarakanisha bunge?
Balozi Kagasheki ambaye hakuulizwa swali lolote ni mbunge wa sasa akiomba ridhaa kwa mara nyingine,
amesema hana malalamiko na mchakato, ameshukuru wananchi kumpendekeza kuendelea kugombea lakini akitaja miradi mbalimbali aliyofanya huku kubwa akiwaomba wananchi wasiendeleze migogoro kuwa haki yao itapatikana kwa mujibu wa taratibu za nchi. 




Bi Eriet ameomba kuwasaidia wananchi kwani akina mama wana huruma huku akisema kuwa mama
mwenye mimba hajui atajifungua mtoto gani, naye hajajua atafanya nini juu ya wananchi lakini wamchague ataleta maendeleo.






Mzee Joseph Kaijage, anasema yeye ni Born here here die here here, hivyo wampe kura hata ikitokea mambo yameharibika hawezi kuwakimbia wananchi watakaa na kutatua pamoja.

Yeye amezaliwa hapaha hapa na atafia hapa hapa hivyo matatizo ya wananchi anayajua na yuko tayari kuyatatua, lakini hawezi kuyatatua bila nguvu ya wananchi hivyo wamuunge mkono kumpa kura.




Bi Selestine Lwezaura, yeye ni mmoja wa akina mama aliyefanya kazi maeneo mbalimbali, hivyo amesema
kazi ya ubunge anaweza kuifanya kusaidia jamii kama wengine au kuzidi wengine, hivyo anaomba ridhaa ya wananchi ili apeperushe bendera na atajitahidi kuwainua akina mama.






Philbert Katabazi (Nyerere) anasema kuwa yeye amependekezwa katika ngazi mbalimbali za uongozi wa
CCM hivyo naye ameamua kujiotokeza kuomba nafasi, kwani wanaopendekeza mara kwa mara wanahittaji kuona naye akijitutumua.






Mjuni Kataraiya akiwa ni mwenye kuomba tena nafasi ya ubunge, akiwa na kumbukumbu ya kuongoza jimbo la Bukoba mjini kama Mbunge mwaka 1995-2000, ambapo anasema alikosea kidogo akafungwa goli.
Alipoulizwa ni nini wananchi wawiwe kumrudisha akasema anglau nilitoa lifti kwa wale waliokuwa watu wazima wakati huo.
Na Mwanaharakati.

Tuesday 28 July 2015

HOTUBA YA EDWARD LOWASA AJIUNGA NA UKAWA KUPITIA CHADEMA

Ametangaza hayo kutpitia mkutano wa UKAWA kupitia vyombo vya habari huku akisema kuwa mabadiliko siyo lazima yapatikane ndani ya CCM hivyo amechukua maamuzi magumu na ametafakari mawazo yake kwa kupitia ushauri wa wanasheria na viongozi kadhaa nchini.

Video itawekwa hapa punde

Na Mwanaharakati.

KAULI YA CCM TAIFA KWA WALIOSHINDWA KULIPIA KAMPEIN BUKOBA



. Ni watatu manispaa ya Bukoba,
. Waitwa wasioridhika,
. Kadi feki zahusishwa.


Dar/mikoani. Michango ya kampeni za kujinadi kwa wananchi katika majimbo mbalimbali nchini imelalamikiwa na baadhi ya wanachama wa CCM wanaowania kuteuliwa kugombea ubunge.

Kutokana na ukali wa michango hiyo, baadhi ya wagombea wamelazimika kujitoa katika mchakato, wengine wakisema hawawezi kumudu kulipa fedha hizo kwa maelezo kwamba ni kiwango kikubwa. Michango hiyo inatofautiana baina ya jimbo moja na jingine.

Hata hivyo chama hicho kimesema hakitishwi na wachache wasioridhishwa na uamuzi unaofanywa kwa masilahi mapana ya chama hicho.

Akizungumzia malalamiko hayo jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema: “Tunaendelea na mchakato wa kura ya maoni. Kila mtu yuko bize na kura, siwezi kuzungumzia watu wachache wasioridhika wakati wengi wanaendelea na utaratibu tuliojiwekea.”

Wagombea watatu katika Jimbo la Bukoba Mjini wamelalamikia kuchangia gharama hizo ambazo kwa mujibu wa agizo la Kamati ya Siasa ya Wilaya, kila mmoja anatakiwa kutoa Sh2 milioni hadi ifikapo leo kabla ya kuanza kwa kura za maoni Agosti Mosi.

Mmoja wa wagombea hao, George Rubaiyuka alidai kuwa kiasi hicho ni kikubwa na kwamba alikuwa tayari amelipa Sh200,000 huku mgombea mwingine, Dk Anatory Amani akiomba aongezewe muda ili akamilishe malipo hayo.

Mgombea mwingine ambaye hajakamilisha malipo hayo ni Mujuni Kataraiya ambaye pia alipendekeza Kamati ya Siasa kuangalia upya kiwango kilichowekwa.

Aliyekuwa mgombea ubunge katika Jimbo la Chalinze, Imani Madega amekaririwa akisema hataweza kukamilisha ndoto yake ya kuwatumikia wananchi wa jimbo hilo kutokana na gharama kuwa kubwa.

Kadhalika, mgombea ubunge Jimbo la Morogoro Mjini, Simon Berege alisema kikao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya kilikutana Julai 21 na kuchanganua gharama za uchaguzi na kila mgombea alitakiwa kulipa Sh6.9 milioni siku hiyohiyo tena zikiwa taslimu.

Berege alisema baada ya uamuzi huo aliomba kupewa muda hadi siku ya pili kukamilisha lakini mgombea mwenzake alijitolea kumkopesha jambo ambalo hakuliafiki.

“Ninaamini ukubwa wa gharama iliyowekwa na sharti la kutokushiriki kwenye kampeni hizo isipokuwa tu kwa kulipa fedha hiyo yote ama kwa awamu mbili na kuzuia mtu kufika kwenye mikutano ya kampeni kwa usafiri binafsi umefanywa kwa makusudi ili kufanikisha nia ile ya awali ya kuwa na mgombea mmoja,” alisema Berege.

Alisema katika mikutano ya kampeni ambayo amekuwa hahudhurii, imekuwa ikitolewa taarifa kuwa amejitoa jambo ambalo si sahihi na kwamba amekuwa akiwasiliana na mkurugenzi wa uchaguzi wa chama akimweleza kuwa anaendelea kufanya jitihada za kutafuta fedha huku akitaka jina lake liendelee kutajwa katika mikutano ya kampeni.

Katibu wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini, Kulwa Milonge alisema hakuna mizengwe ya aina yoyote inayofanyika na kwamba chama kinamtambua Berege kuwa ni mgombea kwa kuwa fomu yake imejazwa kwa usahihi.

Alisema Berege haonekani katika kampeni za kujitambulisha kwa wanachama na kwamba alipewa muda wa kutafuta fedha zilizotakiwa kwa ajili ya gharama za kampeni hiyo, hawezi kutajwa mpaka atakapoonekana katika kampeni.

Kadi feki zalalamikiwa
Huko mkoani Mbeya, wagombea ubunge wa jimbo jipya la Busokelo ambalo awali liliitwa Rungwe Mashariki, juzi wakiwa kwenye Kata ya Lufilyo walitaharuki baada ya kukamatwa kwa kadi 900 za CCM zilizodaiwa kuingizwa kwenye kata hiyo kwa lengo la kumpendelea mmoja wa wagombea.

Hata hivyo, Katibu Msaidizi CCM Wilaya ya Rungwe, Simon Yawoo alisema kadi hizo zilitolewa kwa wanachama waliokuwa wakizihitaji kwenye kata hiyo na kwamba ni halali.

Dk Mahiga alia rushwa
Aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk Agustino Mahiga amekitaka chama hicho na Serikali kushughulikia tatizo la rushwa linalojitokeza wakati wa huu wa uchaguzi kwa uzito unaostahili kwa kuwa vitendo hivyo vinashusha heshima ya chama hicho tawala na kuchafua taswira ya nchi kimataifa.

Dk Mahiga ambaye sasa ni mmoja wa makada 13 wa CCM wanaoomba kuteuliwa na chama hicho kugombea ubunge Iringa Mjini, aliwataka wananchi kushiriki katika vita hiyo ya rushwa na ufisadi katika kipindi hiki cha uchaguzi ili kusaidia kuwapata viongozi bora watakaoongoza na kuliletea tija Taifa.

Na Mwananchi.
 

BREAKING NEWS!!! BUS LA SABUNI LAPATA AJALI MISENYI KAGERA ABIRIA WAPOTEZA MAISHA



. Mapadre watajwa kupoteza maisha,
Kutoka Karagwe kwenda Bukoba limegongana na Cluiser iliyokuwa na mapadre na sisita katika eneo la Bugorora nje kidogo ya Kyaka wilayani Misenyi mkoani Kagera.

Basi hilo nambari za usajiri T650 BFI na Cluiser T166 AGU ambapo waliotajwa kupoteza maisha kwa taarifa za awali ni Padre Onesmo Kahabwa na Michael Mwelinde pamoja Sista Magret Tadebe ambao ni wa parokia ya Katoke waliokuwa wakitokea Lurenge wilayani Ngara.

Tutakuletea undani wa habari hivi punde.
 

Na Mwanaharakati.

ANAYETUHUMIWA KWA UJAMBAZI SUGU BUKOBA AKAMATWA MWANZA

. Anatajwa kuiba milioni zaidi ya 100,
. Amekamatiwa Dar aletwa kwa ndege chini ya ulinzi mkali.
Mtuhumiwa katikati ndani ya gari
Ametajwa kwa majina Ibrahimu Ismail Kingu, ambaye ametuhumiwa kuiba fedha za mfanyabiashara mmoja katika manispaa ya Bukoba, ambapo zaidi ya milioni 140 ziliibiwa baada ya walinzi kunyweshwa vitu vilivyosadikiwa ni sumu.

Fuatilia picha tangu aliposhushwa uwanja wa ndege hadi kufikishwa kituo cha polisi Bukoba.

Sunday 26 July 2015

HUMPHREY POLEPOLE, AWAGUSA WANA-BUKOBA



Ni baada ya kuwataka wananchi kuwa makini na watangaza nia wanaoomba nafasi kupambana na ufisadi ilhali hawana nyezo ya kufanya hivyo.
Hatahivyo wametakiwa kutowasikiliza wagombea wanaojipambanua na vyama, kwani hakuna mfumo wa mgombea binafsi, hivyo wazingatie utendaji wa mtu kupitia chama husika, kwani kumekuwa na wagombea kujinadi wakitaja mambo yanayowakera watanzania, pasipokuonesha njia ya kuyaondoa.

Amesema kuwa kwa sasa wapo wengi wanaotafuta nafasi za uongozi, hivyo vyama husika, vipitishe mgombea kulingana na utekelezaji wake, huku akisema kuwa kisithubutu kupitisha mgombea anayenyooshewa kidole kwani ni kupoteza haki ya wananchi
Akizungumza katika mdaalo ulioandaliwa na taasisi ya mwalimu Nyerere mkoani Mtwara, mwanasheria na mchokoza mada Awadh Alli Said, amesema kuwa wapo viongozi ambao wameshadharau jamii katika nafasi nyingine huku wanajinadi kuwaongoza katika ngazi za juu zaidi, kuwa huko siyo kujenga amani.
Wakati huo huo Bwana Awadh, amewataka wananchi kutumia nafasi yao hadimu ya kuchagua, kumchagua kiongozi anayeonesha njia ya kutetea maslahi yao, kwa kuhepuka wanaotafuta nafasi, huku wakitajwa katika tuhuma za kudhulumu mali zao.

Mdaalo huo ulioandaliwa na taasisi ya Mwalimu Nyerere, unafanyika katika kipindiu amacho mchakato wa kuwapata wa wagombea kupitia vyama mbalimbali ukiendelea kote nchini, huku baadhi ya watia nia wakifukuzwa na wananchi kama ilivyo katika manispaa ya Bukoba ambapo baadhi ya watia nia wanazomewa na wananchi wakihusishwa na uporaji wa ardhi zao. 

Na Mwanaharakati.