MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 26 July 2015

HUMPHREY POLEPOLE, AWAGUSA WANA-BUKOBA



Ni baada ya kuwataka wananchi kuwa makini na watangaza nia wanaoomba nafasi kupambana na ufisadi ilhali hawana nyezo ya kufanya hivyo.
Hatahivyo wametakiwa kutowasikiliza wagombea wanaojipambanua na vyama, kwani hakuna mfumo wa mgombea binafsi, hivyo wazingatie utendaji wa mtu kupitia chama husika, kwani kumekuwa na wagombea kujinadi wakitaja mambo yanayowakera watanzania, pasipokuonesha njia ya kuyaondoa.

Amesema kuwa kwa sasa wapo wengi wanaotafuta nafasi za uongozi, hivyo vyama husika, vipitishe mgombea kulingana na utekelezaji wake, huku akisema kuwa kisithubutu kupitisha mgombea anayenyooshewa kidole kwani ni kupoteza haki ya wananchi
Akizungumza katika mdaalo ulioandaliwa na taasisi ya mwalimu Nyerere mkoani Mtwara, mwanasheria na mchokoza mada Awadh Alli Said, amesema kuwa wapo viongozi ambao wameshadharau jamii katika nafasi nyingine huku wanajinadi kuwaongoza katika ngazi za juu zaidi, kuwa huko siyo kujenga amani.
Wakati huo huo Bwana Awadh, amewataka wananchi kutumia nafasi yao hadimu ya kuchagua, kumchagua kiongozi anayeonesha njia ya kutetea maslahi yao, kwa kuhepuka wanaotafuta nafasi, huku wakitajwa katika tuhuma za kudhulumu mali zao.

Mdaalo huo ulioandaliwa na taasisi ya Mwalimu Nyerere, unafanyika katika kipindiu amacho mchakato wa kuwapata wa wagombea kupitia vyama mbalimbali ukiendelea kote nchini, huku baadhi ya watia nia wakifukuzwa na wananchi kama ilivyo katika manispaa ya Bukoba ambapo baadhi ya watia nia wanazomewa na wananchi wakihusishwa na uporaji wa ardhi zao. 

Na Mwanaharakati.

No comments: