MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday 30 June 2015

KUSINGIZIA MAAFA KWA UZEMBE WA WATENDAJI TANZANIA, KWAVURUGA WIZARA



. Misaada yachelewa na kutolewa kwa wasiowalengwa,
. Taarifa za maafa zapotoshwa serikalini,
. Watendaji serikali watajwa kuvunja taratibu,
. Sheria rasmi yaandaliwa, baada ya kukiukwa taratibu zilizopo.

Kumekuwa na matukio mbalimbali nchini yanayotajwa kuwa maafa, jambo linalosababisha lawama kwa mamlaka wahusika wanapokosa msaada, baada ya kufanyika tathmini na kubainika kuwa siyo maafa kama wanavyokuwa wakidhaania.
Hatahivyo serikali imejikuta ikipoteza muda na kuwa na muingiliano na wadau wa kusaidia jamii, huku ikishindwa kug’amua aina ya maafa kwani kila linapotokea jambo jamii hufikiria kuwa ni maafa, ambapo hayo yote yanasabishwa na ukosefu wa kitengo cha mawasiliano katika ofisi ya waziri mkuu, kama anavyofafanua Benedict Kisaka mratibu wa maafa ofisi ya waziri mkuu.
Ukiukwaji wa taratibu za taadhali ni moja ya sababu zinazoongeza uwepo wa matukio ya majanga na hasa ujenzi holela unatajwa kuwa sababu kubwa inayosababisha mafuriko katika makaazi ya watu, ambapo imebainika kuwa wengine wanajenga kwa maelekezo ya maofisa ardhi na mipango miji.

Bi Naima Mrisho ni kaimu mkurugenzi msaidizi idara ya uratibu wa maafa katika upande wa mipango na utafiti wa ofisi ya waziri mkuu.
Kama kaimu mkurugenzi wa mahafa katika ofisi ya waziri mkuu, nasisitiza hakuna kuendelea kuona watendaji katika taasisi mbalimbali, wanatekeleza kinyume taratibu za nchi, na ndiyo maana tumependekeza kuwa na sheria ya kusimamia maafa ambayo itakwenda sambamba na usimamizi wa kuruhusu watu kujenga katika maeneo yenye utata.

Nakiri kwamba wengi wa wanaojenga kwenye vyanzo vya maji, mabondeni na hata kujenga pasipokufuata mfumo wa kitaalamu wanatokana na mamlaka kuwapa maeneo hayo, sasa tutasimamia sheria .


Januari 2014, yalitokea maafa Kilosa mkoani Morgoro ambapo taarifa iliyosomwa kwa rais na aliyekuwa mkuu wa mkoa huo Joel Nkhaya Bendera ilikuwa kinyume ikilinganishwa na hali halisi ya maafa, ambapo aliamuru warudie kufanya tathmini, jambo linalotajwa kuwa ni athari za ukosefu wa kitengo cha mawasiliano ya maafa wizarani.

Na Mwanaharakati.

UTATA WA KIFO CHA MWANDISHI EDSONI KAMUKARA KATIKA MAZIKO YAKE MULEBA

. Yatajwa kufariki baada ya kukosa hewa,


Edson Slavatory Kamukara, amezikwa kijijini kwao Ihangiro wilayaniMuleba, huku akiacha majonzi kwa familia yake, baada ya kuacha mtoto mmoja ilhali mama yake akisumbuliwa na kupooza, ambapo siku chache zilizopita, Edson alitokea Muleba kumuangalia mama yake, kama alivyozungumza dada wa marehemu aliyejulikana kwa jina la Joyce.

Akizungumza katika maziko hayo, mkurugenzi wa kampuni ya mwana halisi publishers LTD Bwana Said Kubenea, amesema kifo cha marehemu Kamukara, kimezua utata kutokana na hakuna anayejua undani,
huku akisema kuwa madakatari wanasema inaonekana alikufa baada ya kukosa hewa huku, chumbani kwake kukikutwa na damu, akiongeza kuwa alikuwa anakamilisha kazi ya uandishi uliokuwa ukiwahusu vigogo na kama habari zake zingetoka, saizi nchi ingekuwa inaongea mambo mengine.




Waadishi kutoka chama cha waandishi  habari mkoani Kagera KPC, walishiriki maziko hayo na ndiyo walihusika kubeba mwili wa marehemu na picha chini ni Charles Mwebeya akitroa rambirambi yao kwao dada Joyce ambaye anaishi Dar na alikuwa karibu na marehemu.
Marehemu Edson Kamukara, ameacha mtoto anakadiriwa kuwa na miaka kati ya 3 hadi 4 aitwaye  Edigar Ishengoma, na marehemu alianzia kazi ya uandishi katika gazeti la Majira, akafanya jambo leo, tanzania dai, na hatimaye mwanahalisi publishers ambapo amefanyia kwa kipindi cha miezi minne, na alikuwa anakamilisha habari kuhusu matatizo ya wananchi kupitia viongozi mkoani Kagera.
Na Mwanaharakati.

Saturday 27 June 2015

UCHAGUZI WAFANYIKA KAGERA, WAKIUKAJI WASIMAMISHWA UANACHAMA.



. Ni katika tasni ya habari uchaguzi wa kisheria,
. Vinaja watawala uongozini,
. Tetesi za kuvuruga za sikika.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi uliofanyika leo, katika Manispaa ya Bukoba, Msimamizi wa Uchaguzi huo, Padre PROCESSUS MUTUNGI, amesema kuwa bwana MBEKI amepata kura 19,  na kuwashinda JOHN RWEKANIKA na PRUDENCE KIBUKA, ambao wamepata kura tano kila mmoja.

Katibu Mtendaji ni PHINIAS BASHAYA, na katibu Msaidizi ni NICOLAS NGAIZA,  ambao   hawakuwa na mpinzani.
Mweka Hazini ni LILIAN LUGAKINGIRA, ambaye amepata kura 22 na kumshinda AYOUB MPANJA,  ambaye amepata kura saba
Wajumbe wa Kamati  Tendaji ni LIVINUS FERUZI, MATHIAS BYABATO, RAMA MASELLE na JUHUDI FELIX.

Wakati huo huo, Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Kagera-KPC, kimemsimamisha Uanachama kwa Muda, AUDAX  MUTIGANZI,  kwa kukiuka Maadili ya Uandishi wa Habari, huku akitajwa na kuhusika isiyo stahiki ndani ya chama hicho, ambaye hatahivyo alipopewa nafasi ya kujitete alisema yafuatayo.

Na Mwanaharakati.