MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday 27 May 2017

WATANO WAHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA MKOANI KAGERA.




Mahakama kuu kanda ya Bukoba chini ya Jaji mfawidhi wa mahakama kuu kanda ya Bukoba Mh.Salvatory Bangole  imewahukumu watu watano wa wilaya ya Karagwe na Kyerwa mkoani Kagera kutokana na kukutwa hatia ya mauaji.


Wakili wa serikali mkuu na mfawidhi wa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali mkoa wa Kagera Hashimu Ngole amesema kuwa tarehe 24 may mwaka huu walianza kikao cha kesi za mauaji ambazo kimsingi husikilizwa na mahakama kuu,na leo kikao hicho ndo kimefikia hatima yake.

Aidha amesema kuwa kupitia kesi tisa walizokuwa wanasikiliza leo wamefanikiwa kukamilisha saba,kesi moja mshitakiwa alikufa na kesi nne zimetolewa maamuzi.

Kesi ya kwanza ilikuwa na washitakiwa wawili Dastan Makwaya na Jovith Mutagaywa John ambapo walikuwa wanashitakiwa kwa kosa lililofanyika june 17 mwaka 2013 la kumuua Oscar Martin mkazi wa kijiji Kagenyi wilaya ya Kyerwa kwa kumchoma kisu kifuani, watuhummiwa hao wamekutwa na hatia na mahakama imewahukumu kunyongwa hadi kufa.

Kesi ya pili ilikuwa na washitakiwa watatu,Oswald Wilibard,Vicent Clement na Kato simon ambapo walikuwa wanashitakiwa kwa kumuua Elizeus Edimund wa kijiji Kabare wilaya Karagwe mnamo june 16 mwaka 2016,walimfunga kamba mikononi,tumboni na miguuni kisha wakamuning’iniza mpaka kufa na baada ya mahakama kupitia ushahidi imewahukumu wawili kunyongwa hadi kufa ambao ni Vicent Clement na Kato Saimon,pia Oswald Wilbard ameachiwa huru baada ya kuonekana hana hatia.

Kesi ya tatu ilikuwa na mshitakiwa mmoja Ilida Innocent ambaye alikuwa anashitakiwa kwa kumuua mme wake Innocent Kiiza kwa kula njama na majambazi ambao walimkata mapanga mpaka akapoteza maisha,naye amehukumiwa kunyongwa hadi  kufa.

Na kesi ya nne ilikuwa na mshitakiwa mmoja Nuriath Mzakiru ambaye alikuwa anashitakiwa kwa kumuua mme wake Mzakiru Mohamed wa kijiji Kibwera wilaya ya Karagwe mnamo july 26 mwaka 2013,alimuua kwa kumpiga na shoka kichwani, kumkata sehemu zake za siri na kumumwagia maji ya moto,na mahakama wakati ikiendelea na kesi yake alionekana kama mwendawazimu na amewekwa gerezani mpaka siku ukitokea msamaha wa Rais.

Kwa upande wake wakili wa washitakiwa Jackline Mlema amesema kuwa aliteuliwa kufanya kazi ya kuwatetea washitakiwa hao na amefanya kazi kwa uaminifu huku akisema kuwa kufatia hukumu iliyotolewa bado kuna safari ya kukata rufaa katika mahakama ya rufaa ambayo itatenda haki na kutoa notice .


Mahakama kuu kanda ya Bukoba chini ya Jaji mfawidhi wa mahakama kuu kanda ya Bukoba Mh.Salvatory Bangole  imewahukumu watu watano wa wilaya ya Karagwe na Kyerwa mkoani Kagera kutokana na kukutwa hatia ya mauaji.


Na Mwanaharakati.

No comments: