MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 25 May 2017

WANANCHI WAUNGA MKONO UJENZI WA SHULE YA “A Level”BUKOBA VIJINI





Baadhi ya wananchi katika kata ya Rubale iliyopo halmashauri ya wilaya Bukoba wameungana na serikali katika kuwezesha kata yao kupata shule ya serikali kwa kidato cha tano na sita jambo ambalo wanaamin litawasaidia kuinua kiwango cha elimu katika maeneo yao.

Wakiongea macmedianews.blogspot.com,wamesema kuwa wamejitoa kuchangia mchanga,matofali,mawe na kokoto kwa kila kaya inayojiweza huku wakiiomba serikali kuwaunga mkono kwa kuwanunulia vifaa vya madukani  ili kuhakikisha wanakamilisha kwa muda uliopangwa.

Kwa upande wake afisa mtendaji wa kata Rubale Bw.Abdala Rwabigimbo amesema kuwa muitikio wa wananchi ni mzuri lakini wameshirikisha kata za jirani kwa ajili ya kuongeza nguvu maana wanataka ujenzi uanze rasmi mwezi wa sita.

Aidha ameongeza kuwa wana mpango wa kujenga mabweni,jiko na bafu maana madarasa ya kutumia tayari yapo,huku akisema kuwa kwa upande wa fedha ipo million mbili ya kuanzia na serikali ipo mbioni kuwaunga mkono.

Diwani wa kata Rubale Stanslaus Rutta amesema kuwa mradi huo wameshauombea fedha lakin hazijapatikana ila wanasubili kikao cha bajeti cha bunge kiishe ili waweze kupata hizo fedha zitakazounganishwa na nguvu za wananchi ili kufanikisha ujenzi huo


Na Mwanaharakati.

No comments: