MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday 11 October 2014

TAARIFA KAMILI NA PICHA KUHUSU KUKWAMA KWA MELI YA MV VICTORIA NA KUZUA RAPSHA KWA ABIRIA NA JAMAA ZAO BUKOBA

Meli hiyo iliyoondoka katika bandari ya Bukoba jana usiku,  mfuko wake wa kuendeshea meli ulishindwa, ikiwa zimebakia maili kadhaa kabla ya kufika katika bandari ya Kemondo.


Kapteni wa meli hiyo, Bempele Samson amesema kuwa mfumo wa meli hiyo ulishindwa ikiwa majini kabla ya kufika katika bandari ya Kemondo  na kulazimika kutumia mfumo wa mbadala ili kuiwezesha kufika katika bandari hiyo.
Naodha wa meli hiyo Bwana Samson akihojiwa na mtandao huu.


Wakizungumza na mtandao huu, baadhi ya abiria hao wamesema kuwa kushindwa kwa mfumo huo , kuliibua hofu kubwa miongoni mwa abiria na kufanya baadhi yao kuanza kuangaika.


Abiria hao wameitaka serikali  kupitia kwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Kikwete kutekeleza ahadi yake ya kununua meli mpya aliyoitoa wakati wa kampeni za uchagunzi mwaka 2010.

Picha juu na chini ni abiria pamoja na mizigo yao kama ndizi mbivu na mbichi ambazo wanasema kuwa zitaharibika kabla ya kufika Mwanza.


Afisa SUMATRA mkoani Kagera Bw Alex Katama, ametueleza kuwa mpaka sasa wamemsubiri fundi kutoka bandari ya Mwanza ili kufanya marekebisho ya mfumo wa meli hiyo, huku akisema kuwa unafanyika utaratibu wa kurudidha nauli za baadhi ya abiria ambao wameondoka na usafiri mwingine, huku wengine ambao hawataki tena kusafiri watarejeshewa pia  pesa zao za nauli.
Na Mwanaharakati.

1 comment:

nyh said...

Shocked. How can this happen repeatedly? We need explanations from the responsible government leaders. Probably, from Hon Mwakyembe and his deputy Hon Tizeba. They must tell us what went went wrong and why? I still remember that darkest day when Mv Bukoba capsized. It was one of the darkest day i will never forget. We lost our loved ones, brothers, sisters, fellow staff members, neighbours, and all what one can mention . Please, please, tell us why this is reminding us tbe event in the same generation?