MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday 27 May 2017

WANAFUNZI WATAHABIKA MASHINDANONI, RAS AAGIZA HATUA ZA HARAKA KWA HALMASHAURI KUTOA FEDHA.



MULEBA 
                                                                                                                                          

Mashindano ya michezo kwa  shule za sekondari{UMISETA}yamezinduliwa rasmi katika chuo cha uwalimu katoke mkoani Kagera kwa kushirikisha wilaya zote za mkoa wa Kagera zikiwa na jumla ya wanamichezo 469.

Akiongea mbele ya mgeni rasmi,Afisa elimu mkoa Kagera Aloyce Kamamba amesema kuwa wanaoshiriki michezo ni jumla ya wanamichezo 469,walimu na maafisa elimu 40,wanafunzi ni wasichana 192 na wavulana 277 huku akisema kuwa hatua ya kwanza itakamilika may 29 mwaka huu na kupata timu moja ya mkoa itakayokuwa na wanamichezo 91 na walimu 15.

Aidha amesema kuwa may 30 mwaka huu timu hiyo itaanza kambi mpaka june 4 ambapo june 5 itareport chuo cha uwalimu Butimba jijini mwanza kwa ajili ya kushiriki mashindano kitaifa ambayo yanatarajia kukamilika june 17 mwaka huu.

Pia Kamamba amesema kuwa changamoto kubwa wanayokumbana nayo ni pamoja na baadhi ya halmashauri ukitoa ya Bukoba,Karagwe na Kerwa zimeshindwa kukamilisha michango yao kifedha kwa ajili ya kuendesha mashindano hayo hali inayosababisha baadhi ya vitu kukwama.

Akizindua mashindano hayo,Katibu tawala mkoa wa Kagera Kamishina wa polisi Diwan Athuman ametoa siku tatu kwa wakurugenzi wa  halmashauri zote ambazo hazijakamilisha michango hiyo kuhakikisha wanazitoa ndani ya muda huo na apate mrejesho wao.

Sanjali na hayo amewasihi wanamichezo kufanya vizuri katika mashindano yao ili kuhakikisha mkoa wa kagera unafanya vizuri hatua ya kitaifa itakayoanza june 5 mwaka huu.



Na Mwanaharakati.

No comments: