MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 28 May 2017

PICHA 5;ILIVYOZINDULIWA WIKI YA MAZIWA KITAIFA


 
Akizindua shughuli hiyo Naibu waziri wa Kilimo,mifugo na uvuvi mh.William Ole Nasha amesema kuwa nchi ya Tanzania ina changamoto kubwa kwa upande wa matumizi ya maziwa ambapo kwa mwaka mtanzania mmoja anatumia wastani wa lita 47 ambayo ni chini ya robo ya kiwango kinachopendekezwa na shirika la afya duniani badala ya lita 200,hali aliyosema inasababisha hata kuendelea kwa kiwango kikubwa cha udamavu kwa Watanzania.

Pia amewasihi wananchi kuhudhuria kwa wingi katika kipindi hiki cha wiki ya maziwa ili waweze kupatiwa elimu ya kutosha juu ya matumizi ya maziwa ikiwa ni pamoja na kutambua magonjwa unayoweza kupata usipokunywa maziwa.



Wiki ya maziwa kitaifa  imezinduliwa leo mkoani kagera katika viwanja vya Kyakairabwa vilivyopo ndani ya manispaa ya Bukoba ambayo itafikia kilele  june 1 mwaka huu,ikiwa na lengo la kutoa elimu kwa wananchi juu ya matumizi ya maziwa.








Na Mwanaharakati.

No comments: