MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 28 August 2014

DC BUKOBA AKABIDHI BAISKELI KWA WAJASRIAMALI WANANWAKE MANISPAA YA BUKOBA.

 Kikundi cha Wanawake Wajasiriamali, kinachojihusisha na Usindikaji wa vyakula manispaa ya Bukoba kimepatiwa wa Baiskeli 39 ili ziweze kuwasaidia Wajasiriamali hao katika shughuli zao za uzalishaji.


                                     
 Picha juu ni Bi Ziporah Pangani, mkuu wa wilaya Bukoba, akipewa maelezo na mratibu wa kikundi Bi Jesca Jonathan, alipowasili kwenye ofisi yao.
 
 Akikabidhi Baiskeli hizo, mkuu wa wilaya ya Bukoba , ZIPORAH PANGANI amewahimiza wanawake hao kuendelea na umoja huo,  kwani kupitia kikundi hicho wameweza kufanya shughuli zao za kimaendeleo.


Akisoma risala ya wana kikundi,  Mratibu wa kikundi hicho JESKA JONATHAN amesema kuwa, kikundi kina jumla ya wanachama 425 ambao wamekuwa wakijihusisha na shughuli za kilimo na usindikaji vyakula.

Na Mwanaharakati.

No comments: