MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday 19 October 2011

                                                            PORINI BUZIKU(CHATO)
Kumekuwa na taratibu za kukataza ukataji wa mkaa katika misitu ya hifadhi mkoani kagera lakini wakti huo mkoa huu ukiwa ni ule unaoongoza kuwa na gharama kubwa katika upatikanaji wa nishati mbadala.

Buziku ni moja ya misitu ya hifadhi ambayo imehifadhiwa kwa ajili ya mimea kitaifa lakini kwasasa ni sehmu ambayo imeshambuliwa na ukataji wa mkaa kwa kiasi kikubwa pamoja na uchungaji wa mifugo na kilimo katika msitu huo.

Kwenye picha huo ni baadhi ya magunia ya mkaa ambayo yameshuhudiwa na mtaalamu wa habari hizi wakti huo akiongea na wahusika wakasema kuwa wanafanya hivyo kwasababu ya maisha magumu.

Kwaupande wake afisa mali asli wa wilaya ya Chato bwana CHARLES SALEHE anasema msitu unapunguwa kwa kiasi kikubwa lakini wao kama wahusika wanakabiliwa na vitendea kazi ili kufanya doria za kutosha na baadhi ya wanasiasa wanahusika kuwadanganya wavamizi hao kwa kisingizio cha kuwapigia kura.

No comments: