MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday 28 November 2014

WAWEKEZAJI WAVUTWA GEITA



Na Valence Robert Geita.
28.11.2014.
WAWEKEZAJI Mkoani Geita  wametakiwa kuwekeza kwa  wingi kwenye  Mkoa huo ili  vijana  walioko kuweza kupata ajira  kuliko kwenda kuwekeza kwingine na kuwanufaisha wasiokuwa wazawa wa Mkoa husika.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Geita Manzie Mangochie wakati wa kufungua KG Hotell iliyoko katika  mtaa wa misheni  kata ya kalangalala Wiyani Geita Mkoani hapa iliyojengwa na mfanyabiashara mzawa.

Mangochie alisema kuwa wafanyabiashara  Mkoani Geita wamekuwa wakienda kuwekeza Mikoa mingine au nchi za nje na kuwanyima haki ya kupata ajira vijana wazawa hivyo kuwaomba kuendelea kuwekeza katika mkoa huwo  ili na maendeleo yazidi kukua kwa kasi.

Jamani nawaomba wafanyabishara wa Mkoa huu muwekeze katika Mkoa huu ili vijana wetu waweze kupata ajira kuliko kuwekeza kwingine na ninawaomba kuzingatia kama kazi uliyo nayo inaweza kufanywa na watu wa Mkoa huu sioni haja ya kwenda kutafuta kwingine maana kuwapa ajira wazawa nanyi mnaongezewa zaidi alisema Mgochie.


Na Mwanaharakati.

No comments: