MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 25 July 2013

RAIS KIKWETE AMEWAAHIDI WANANCHI WILAYANI MULEBA KUPIMA ARDHI NA KUONDOA MGOGORO KWA WANAOPAKANA NA KAMBI YA KABOYA.

 Mheshimiwa Mwijage, amesema kuwa mgogoro wa wananchi na kambi ya Kaboya, aueleweki kutokana na kutokuwapo mipaka ya kambi hiyo, kitendo kinachosababisha wananchi washindwe kutumia ardhi kutokana na masuala ya ulinzi na usalama, ilhali jeshi nalo linatakiwa kuheshimia.
 Katika hatua nyingine, mbunge huyo amesema kuwa wananchi wakabiliwa na ukosefu wa huduma ya umeme, ambapo walishapewa ahadi ya kupatiwa huduma hiyo kupitia REA, lakini hadi sasa hakuna kilichoishatekelezwa na kusababisha lawama kwa viongozi wa jimbo hilo.


 Rais Kikwete amesisitiza kuwa ulinzi na usalama umeimarika katika mkoa na nchi ya tanzania, kutokana na kauli ya mkuu wa majeshi Jenerali DAVIS MWAMUNYANGE, kuwahahikishia wananchi kuwa jeshi liko imara na linazingatia ulinzi kwa wananchi wake.
 Wananchi wakifuatilia hotuba fupi ya rais wa jamhuri ya muungano Tanzania baada ya kuweka dhana za asili kwenye mwenge wa kudumu ktk makaburi ya mashujaa.

Mbunge wa jimbo la Bukoba mjini Balozi HAMIS KAGASHEKI, akisalimiana na viongozi wengine wa kitaifa katika maadhimisho ya siku ya mashujaa kambini Kaboya.

Rais Kikwete ameendelea na ziara yake mkoani Kagera, ambapo sasa yupo wilayani Muleba ambapo atahutubia wananchi baada ya kuzindua mradi wa maji katika eneo la IYAKO, na bada ya hapo anapumzika na kuelekea Biharamulo.
MWANA HARAKATI

No comments: