MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday, 18 July 2015

BREAKING NEWS!!!MWENYEKITI CCM BUKOBA MJINI AJIENGUA, SIRI IKO HAPA



Nimeamua kuacha kuchukua fomu ya kugombea kwasababu inaonekana wenzangu wana CCM wananitenga, tangu kata yetu ilipopoteza wenyeviti wote wa mitaa katika uchaguzi uliopita.

Ni kauli ya mwenyekiti CCM wilaya na aliyekuwa diwani wa kata Kashai manispaa ya Bukoba Yusuph Ngaiza, ametangaza kutogombea tena nafasi hiyo.

Akizungumza na mwandishi habari wamtandao huu, Bwana Ngaiza amesema kuwa ameongoza kata hiyo kwa miaka 15, ameamua apumuzike huku akiwasihi wana CCM kuwa wamoja ili kuendeleza ushindi ulioanzishwa na waasisi hatimaye kuwaletea wananchi maendeleo.

Ameelezea miradi ya maendeleo iliyofanywa wakati wa uongozi wake, huku akimsihi atakayechaguliwa msimu ujao kuendeleza alichokiacha huku akiwashukuru wa baadhi ya viongozi wa kata hiyo.

Ameongeza kuwa tayari mkandarasi anaendelea na ujenzi wa barabara hiyo na itakamilika mwezi wa nane, hivyo akawataka wananchi kuitunza miundombinu hiyo akisistiza viongozi wao kuendelea kupendekeza miradi kwani Kashai bado ina uhitaji mkubwa wa maboresho.
Bwana Yusuph Ngaiza, anaendelea na nafasi yake ya uenyekiti wa CCM wilaya alipochaguliwa katika nafasi hiyo 2012, na amesema kuwa sasa atakuwa na nafasi nzuri kushughulikia masuala ya kisiasa kwa kuhakikisha anasimamia viongozi watakaochaguliwa ili watekeleze ilani ya CCM.

Alianza udiwani katika kata ya Kashai mwaka 2000 kwa ushindi wa kura 620, na mwaka 2005 aliendelea na nafasi hiyi baada ya kumshinda Khalfan Ramadhani Bahati kwa ushindi wa kura 800 na mwaka 2010 alichaguliwa kwa kuwashinda Ali Kabaju wa CUF , na Lenatus Kilongozi (Ikengya) wa CHADEMA, alipowashinda kwa kura 475. 

Na Mwanaharakati.

No comments: