By Lameck Richard
Walimu 28 kutoka shule za msingi kumi na nne za halmashauri
ya wilaya Bukoba wamekabidhiwa vyeti vya
kuhitimu mafunzo ya semina fupi iliyoanza may 15 mwaka huu ambayo ilikuwa
inaendeshwa chini ya ufadhili wa shirika la JAMBO BUKOBA.
Akikabidhi vyeti hivyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa
halmashauri ya wilaya Bukoba,Afisa Michezo wilaya hiyo Bw,Gosbert Kamuntu amelipongeza shirika la Jambo Bukoba
linaloendeshwa kwa ufadhili wa Clemens Mulokozi
kwa kazi nzuri wanayoifanya huku akiwasihi wazazi na walezi kuruhusu watoto wao
kushiriki michezo kwani michezo ni ajira na ni sehemu mojawapo ya kuendeleza
vipaji vyao.
Kwa upande wake Meneja
Mradi wa shirika la jambo Bukoba Iman Paul amesema kuwa mwaka 2008 walianza
rasmi kutoa semina kwa walimu wa shule za msingi mbalimbali ndani ya manispaa
ya Bukoba na halmashauri ya wilaya Bukoba ambapo kufikia may 19 mwaka huu
wamekamilisha zoezi hilo kwa wilaya hizo mbili,na semina zinaendelea kutolewa
kwa wilaya nyingine zote za mkoa wa Kagera .
Aidha amesema kuwa malengo ya shirika la Jambo Bukoba ni
kuendeleza vipaji vya watoto kupitia michezo ndani ya mkoa wa Kagera kwa kujali
usawa wa kijinsia,kutoa elimu ya ukimwi na elimu kwa ujumla.
Bi,Paul ameongeza kuwa pamoja na kuendesha michezo hiyo
wamejikita pia katika kuboresha miundombinu katika shule za msingi mbalimbali
ndani ya mkoa wa Kagera kujipatia kiasi cha shilingi milioni nne ambazo huzitoa
kwa kila timu inayoshiriki bonanza la mkoa na ufanyika mara moja kwa mwaka.
Kwa upande wa wakufunzi katika semina hiyo mwl William Magesa na Bi,Macleth Joseph{Mrs
Kamuntu}wamewasihi wahitimu wote kuhakikisha wanakuwa balozi wazuri kwa
kuwafundisha wanafunzi wao michezo yote
waliyojifunza kupitia semina hiyo .
Sanjali na hayo,wahitimu wamelipongeza shirika la jambo
Bukoba kwa kuanzisha mafunzo hayo huku wakisema awali walikuwa na changamoto
kubwa kimichezo lakini kuanzia sasa wanahaidi watafanya vizuri zaidi kwa
wanafunzi wao kwa kuwafundisha kile walichokipata ndani ya semina hiyo.
UNAWEZA KUTAZAMA FULL
VIDEO HAPA YA MENEJA MRADI Iman Paul………….....
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment