Rais wa Uganda ambaye ni mwenyekiti mpya wa Jumuhiya ya
Afrika Mashariki EAC, amesema kuwa kuungana ni jambo la msingi lakini siyo kwa
lengo la kuungana kusalimiana au kutakiana hali tu bali kuungana na kutekeleza
mambo ya msingi na yenye kuchochea maendeleo.
Amesema hayo muda mfupi baada ya kukabidhiwa nafasi ya
mwenyekiti wa jumuhiya ikulu jijini Dar es salaam Tanzania, katika kikao cha 18 cha
kawaida cha EAC, ambapo imeasainiwa mikataba mbalimbali ya utekelezaji wa
masuala kadhaa katika nchi sita mwanachama.
Mkutano huo umeudhuriwa na marais wawili ambao ni mwenyeji
Dr. John Magufuli, Yowery Museven wa Uganda, kaimu rais wa Kenya Wiliam Rutto,
na wawakilishi wengine wa marais ya mataifa ya Rwanda, Burundi, Sudan kusini na
Somalia ambaye anaomba kuingizwa kwenye jumuhiya hiyo.
Rais Magufuli ambaye ameongoza jumuhiya hiyo kwa miaka
miwili, amesema kuwa amefurahishwa na maendeleo ya jumuhiya hiyo, hivyo
kumwomba mwenyekiti mpya kuendeleza walichoanzisha viongozi waliowatangulia,
hata kama ni kazi ngumu kuendeleza jumuhiya hiyo.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment