MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 25 November 2012

SIKU MOJA BAADA YA MBUNGE WA BUKOBA MJINI KUSEMA KUWA SOKO LA BUKOBA HALITAVUNJWA MPAKA WATAALAMU WAPIME HALI YA ARDHI YA SOKO, LIMEFIKA GARI LILILOSHEHENI MASHINE ZA KUCHIMBA ARDHI ILI KUPIMA KINA CHA MAJI NA KUFUKUZWA NA WAFANYABIASHARA WA SOKO HILO

Wakizungumza na waandishi wa kituo hiki, wafanyabiashara hao wamesema kuwa hawakubaliani na utaratibu unaofanyika kwasasa kwani unawanyioma ushirikiano, huku wakihamini kuwa vifaa hivyo vimeletwa kwajili ya kufanya tathmini ya kina cha maji katika soko hilo, ili liweze kubomolewa.
Hata hivyo dereva na mafundi waliokuwa na gari hiyo aina ya FUSO yenye nambari za usajiri T 975 AUJ kutoka kampuni ya GEOPINUS ENGINEERING LTD  kutoka Dar es salaam, wamesema kuwa kampuni yao imetambulika na wameletwa na tajiri yao kwa shughuli ambayo hawakupenda kuisema.
Hali hiyo imejitokeza siku moja baada ya mbunge wa jimbo la Bukoba mjini Balozi HAMIS KAGASHEKI, kusema kuwa ili soko livunjwe ni lazima kufanyika upembuzi yakinifu ikiwa ni pamoja na kujua ni kiasi gani cha maji kiko chini ya ardhi ya soko, jambo ambalo mpaka sasa halijafanyika.

No comments: