MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday 21 December 2012

PROFESA TIBAIJUKA AMEITAKA OFISI YA USHURU WA FORODHAS MPAKANI MTUKULA KUHAKIKISHA MAGARI YANAYOEGESHWA MAPAKANI HAPO HAYAKAI KWA MUDA MREFU

Waziri wa ardhi nyumba na makazi  Profesa Anna Tibaijuka, ameitaka ofisi ya ushuru wa forodha mkoa wa Kagera, kuhakikisha inaweka mipango mizuri katika kituo cha mtukula ili kupunguza usumbufu wa watumiaji  wa mpaka huo.
Akizungumza na ofisa fordha wa  kituo cha mtukula bwana PANGANI, Profesa Tibaijuka  amesema kuwa pamoja na kuondoa usumbufu, mkoa utajipatia faida baada ya kufanya shughuli zake kwa haraka.
Ametoa kauli hiyo baada ya kuona mpaka wa mtukula umejaa  magari makubwa ambayo yantoka nchini Uganda, na kusababisha foleni kubwa ambayo hata hivyo inaingiza kiasi kidgogo cha fedha kwani magari hayo yanatozwa shilingi 3000/= tu kwa siku.

 Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa kagera kanali mstaafu FABIAN MASSAWE, amesema kuwa ameshtushwa na na hali hiyo, ambapo amewataka wasimamizi wa ushuru wa forodha kupandisha kiasi cha fedha wanachotoza kwa wenye magari hayo, ili kuongeza pato la mkoa na taifa.

Ameongeza kuwa kiasi cha ushuru kikiwa kikubwa usumbufu utapungua.

Kwa upande wake afisa forodha wa kituo cha mtukula bwana PRIMUS PANGANI, amesema kuwa magari hayo yanalipiwa shilingi elfu 3, na kuwa taratibu zote zinakuwa zimekamilishwa kwa upande wa Tanzania, isipokuwa waganda wanakuwa hawajakamilisha ndiyo maana yanaendelea kuwepo.

MWANA HARAKATI

No comments: