MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday 26 February 2013

BARAZA LA BAJETI LA MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA LASHINDWA KUFANYIKA BAADA YA IDADI YA MADIWANI WANAOTAKIWA KUTOTIMIA



Kikao cha kujadili bajeti cha Baraza la madiwani wa halmashauri ya manispaa ya Bukoba leo kimelazimika kuahirishwa kutokana na sababu ya akidi kutotimia ambapo wajumbe walioudhuria kikao hicho walikuwa 11 kati ya 24.

Mkurugenzi wa manispaa ya BUKOBA Bwana HAMIS KAPUTA  amesema kuwa kwa mujibu wa sheria na kanuni za uendeshaji wa vikao vya alimashauri kikao hicho kisingeweza kuendelea kama wajumbe hawajafika nusu ya wajumbe wote wa kikao hicho.

Kikao cha kujadili bajeti cha  baraza la madiwani kimeharishwa na mstahiki MAE wa manispaa ya Bukoba DR ANATHORY AMANI kwa siku saba na endapo akidi isipokamirika bajeti itajadiliwa na wajumbe watakaoudhuria.

Wakati huo huo muheshimiwa mkuu wa wilaya ya Buoka bi ZIPORA PANGANI amewaomba watumishi wa serikali katika manispaa ya Bukoba kutojiusisha na migogoro ya siasa na kuonyesha itikadi zao sehemu za kazi na kuongeza kuwa atakaefanya hivyo atawajibishwa kwa mujibu wa sheria.

No comments: