MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 28 January 2014

TAKRIBANI WATU 583 WAMEATHIRIKA NA MAFURIKO YA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA KATIKA KATA YA MPUNGUZI MKOANI DODOMA NA KUSABABISHA NYUMBA 146 KUANGUKA .




Diwani wa kata ya  mpunguzi mh john Matonya ameseama pamoja na idadi hiyo ya nyumba zilizo anguka bado nyingine zinaendelea kuanguka .
Aidha mh matonya amesema miundombinu mibovu ndio chanzo cha mafuriko hayo kutokana na kujengwa bila kiwango kizuri.
Hata hivyo mh matonya ameomba miundombinu iboreshwe ili kuondoa adha ya mafuriko wakati mvua zinaponyesha.

WAMILIKI WA MITANDAO YA SIMU   ZA MKONONI  TANZANIA  WAMEELEZA SABABU ZINAZOPELEKEA  WAO KUSHINDWA  KUWEKA  MINARA  YA SIMU KATIKA  MAENEO YA VIJIJINI

Hayo yamejiri mara baada ya wakazi wa kijiji cha solowu wilayani  chamwino kulalamikia ukosefu wa  mawasiliano ya mitandao ya simu  kwa  muda mrefu .

Mfanyakazi wa  mtandao wa  zantel Bw  Brayan Donard amesema   ukosefu wa miundombinu  vijijini ndo sababu kubwa   inayowapelekea wao kushindwa  kuwafikia  wakazi wa  maeneo hayo.

Aidha Bwana Brayani ameongezea kuwa  wana malengo ya kuwafika watanzania wote ila kwa sasa wameanza na wakazi wa Dodoma mjini  na wanaelekea  vijijini.

Sanjari na hayo  amewataka wakazi  wa maeneo ambayo  yamekuwa  yana matatizo ya mtandao  wawe  wavumilivu   kwani wanawakumbuka na muda ukifika watawafikia

DIWANI WA KATA YA CHILONWA WILAYANI CHAMWINO AMEITAKA SERIKALI KUJENGA DARAJA LA CHILONWA LILILOSABABISHA  WATU WATATU KUPOTEZA MAISHA KUFUATIA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA.
Mh Yaledi Sinon  amesema tangu kutokea kwa tukio hilo mpaka sasa hakuna harakati zinazofanyika baada ya meneja wa mkoa kuahidi kutafuta jitihada za matengenezo.

Aidha mh  Sinoni amesema tangu kutokea tukio hilo  mpaka hivi sasa hakuna kiongozi yeyote aliefika  hapo kwa ajili ya kutatua kero hiyo.

Hata hivyo ameomba madereva kuwa makini katika daraja hilo kutokana na kuendelea kunyesha kwa mvua na kuwataka makandarasi kutengeneza daraja hilo.

ZAIDI YA MAGARI 1,000 YAMEKWAMA KWENYE BARABARA KUU YA MWANZA  KWENDA  DAR ES SALAAM KATIKA KATA YA MIGUWA, WILAYANI NZEGA, KUTOKANA UTEKAJI WA MALORI ULIOFANYWA HIVI KARIBUNI.

Madereva wamegoma kuondoa magari yao baada ya kukasirishwa na kitendo cha polisi wa Nzega kushindwa kuwasaidia wakati walipotekwa.

Kutokana na tukio hilo,madereva wamegoma kuondoa magari yao na kusababisha mabasi ya abiria na malori ya mizigo kukwama wakati abiria wapatao 3,000 wakitaabika kwa kukosa chakula na maji.

Aidha Madereva hao wameapa kutoondoa magari hayo hadi Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mathias Chikawe na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Fatma Mwassa watakapofika kwenye eneo hilo ili kusikiliza kilio chao.

Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Nzega, Emmanuel Mihayo amesema watu wamejeruhiwa vibaya kwenye utekaji huo kwa kukatwa masikio na kutobolewa macho.

WATU WANNE WAMEPOTEZA MAISHA KWA KUSOMBWA NA MAJI MKOANI  HAPA , KUTOKANA NA MVUA ZINAZO ENDELEA KUNYESHA NCHINI.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime amesema watu hao wanatoka maeneo tofauti lakini vifo vyao vimetokea kwenye mito inayotiririsha maji kwa msimu.

Katika  tukio la hivi karibuni mkazi mmoja wa kijiji cha Mpinga mwenye umri wa miaka 55 amefariki baada ya kutumbukia kwenye mto Mpinga ambao ni wa msimu.

Kamanda Misime amesema tukio jingine limetokea  mwanzoni mwa wiki iliyopita, ambapo  watu wanne walitumbukia na gari waliyokuwa wakisafiria  katika mto Chinyasungwi, kijiji cha Mahampa, Wilayani  Chamwino na watatu kati yao walikufa huku mmoja akiokolewa.
 

MWANA HARAKATI

No comments: