MWANAFUNZI wa miaka 8 Rachel Isaya wa
darasa la kwanza katika shule ya msingi Nyakabale wilayani Geita, amelishwa
kinyesi chake baada ya kukutwa anajisaidia kwenye kisima akiwa na wenzake
wakitoka shuleni.
Kamanda wa polisi mkoani Geita
Joseph Konyo akizungumza na waandishi wa habari amesema kuwa tukio hili
limetokea tarehe 11 mwezi huu majira ya saa 4 asubuhi wanafunzi hao walipokuwa
wanatoka shuleni kufanya usafi mwanafunzi huyo akiwa na wenzake watatu
ambao hawakufahamika majina yao walipofika eneo hilo Rachel alienda
kujisaidia karibu na kisima hicho cha Marco Maico.
Konyo ameendelea kusema kuwa mara tu
alipomaliza kujisaidia Marco alipita na kukuta kinyesi hicho ambapo alimwamuru
akizoe kwa mkono kinyesi hcho hata hivyo alipoenda kukitupa Marco akamwambia
akile hadi kiishe na kwa hofu ya kutaka kupigwa alikila kinyesi hicho huku
wenzake wakimsubili baada ya kumaliza alienda nyumbani na wenzake.
Baada ya kufika nyumbani mwanafunzi
huyo alimwambia mama yake Agnes Lujaja(26) juu ya kilichotokea na mama yake
akaenda kwa balozi wa nyumba kumi kutoa taarifa ambapo akampa barua ya
kumpeleka zahanati ya Nyakabale kwa matibabu zaidi baadaye balozi huyo alitoa
taarifa kwa Polisi na baada ya mda walifika kwenye eneo la tukio na kumtia
mbaroni mtuhumiwa huyo.
Katika hatua nyingine kamanda
Konyo amesema kuwa Jumanne Joel(25-30) ameuawa na wananchi wenye hasira kali
mara baada ya kumvamia Monica Lutonja(32) wa kijiji cha nyankumbu katika
kata ya kalangalala mjini hapa .
Aidha tukio hilo limetokea usiku nwa
kuamkia leo ambapo inadaiwa kuwa watu watatu akiwemo marehemu walienda kwa mama
huyo na kugonga hodi wakidai kuwa wao na rafiki wa kaka yake ambaye ni Bunegezi
na alipofungua walianza kumkatakata mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake
hadi kupoteza fahamu.
Hata hivyo kelele za mama huyo
zilisababisha majirani kutoka na kuanza kuwasaka baada ya kuwa wamekimbia na
hatimaye wakamkamata mmoja na wakaanza kumpiga hadi kumuua.
Kamanda amesema kuwa watuhumiwa
wengine wawili bado wanatafutwa na jeshi la polisi kwa ajili ya kufikishwa
kwenye vyombo vya sheria.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment