MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday, 6 June 2014

WALIMU 97 WA SHULE MBILI WILAYANI GEITA WATUMIA TUNDU MOJA LA CHOO.



Walimu hao 97 ni wa katika shule ya msingi Nyankumbu na Mkombozi wanatumia tundu moja la choo ambacho kiko kwenye nyumba ya mwalimu, huku wanafunzi 3563 wa shule hizo mbili wakitumia matundu 14, jambo ambalo limekuwa kero.

 Akizungumza na waandishi wa habari shuleni hapo, mwalimu mkuu wa shule ya msingi Nyankumbu Jasmin Ngume, alisema kuwa awali ilikuwa shule moja baadaye imegawanywa na kuwepo Mkombozi shule ya msingi ambapo imeendelea kutumia tundu moja kwa walimu wote huku wanafunzi wakigawana matundu 7 kila shule.
Ameongeza kuwa kwa mjibu wa taratibu za wizara uwiano wa  vyoo walimu wa kiume 4 hutumia tundu moja na walimu wa kike 3 hutumia tundu moja, na wanafunzi wakiume 3 hutumia tundu moja na wakike 4 hutumia tundu moja.

Aidha mwalimu huyo amesema kuwa kumekuwepo na sintofahamu ya namna ya kujisaidia kwa walimu na wanafunzi, kiasi kwamba wamekuwa wakienda kwenye nyumba za majirani na hata kuzuiliwa na kuambiwa kuwa wanavyoo jambo ambalo linawasababishia wakati mwingine kurudi nyumbani ili wakajisaidie huku muda wa kazi ukiwa bado anahitajika shuleni.

Uchunguzi wa mwandishi umebaini kuwa shule hii ya muda mrefu awali ilikuwa ni ya ufundi na majengo ambayo yalikuwepo kipindi cha ufundi ni asilimia kubwa ndiyo yanayotumika kipindi kile huku kwa sasa shule ikipanuka na kuwa na wanafunzi wengi zaidi.

Baadhi ya wanafunzi walioongea na mwandishi wamedai kuwa usumbufu wanaoupata unawasababishia kutosoma kwa raha na wakati mwingine wanahofia kula wakati wanakuwa na njaa kwa sababu itawalazimu waende nyumbani.
  Na Mwanaharakati.

No comments: