Mama mmoja Tecra Kazimili(24) mkazi wa Lubili katika wilaya ya
Misungwi Mkoani Mwanza, amjefungua watoto (4) kwa wakati mmoja huku mtoto mmoja
wa kiume amefariki muda mfupi baada ya mama huyo kujifungua.
Akizungumza
na waandishi wa habari waliofika kushuhudia tukio hilo ambalo si la kawaida, mama Tecra alisema hii ni mara yake ya nne
kujifungua lakini ni mara yake ya kwanza kujifungua watoto wanne kwa wakati
mmoja.
Tecra
ambaye amelazwa katika wodi ya wazazi katika Hospitali ya wilaya ya misungwi
Mkoani Mwanza, alisema anamshukuru Mungu
kwa kumjalia Afya njema na kumuwezesha kujifungua watoto (4) pamoja na kwamba
mmoja wa watoto hao amepoteza maisha muda mfupi baada ya kuzaliwa. “yote ni
mipango ya mungu.”alisema Tecra
Tecra
aliongeza kuwa uzao wake ya nne lakini hana mtoto hata mmoja kutokana na watoto
wake wote (3) kufariki wanapofikisha mwaka mmoja hadi mmoja na nusu kitendo
kilichosababisha kufukuzwa na mume wake Mussa Masalu aliyekuwa anaishi naye
baada ya kuona watoto wanafariki na kudaiwa kuwauwa yeye mwenyewe jambo ambalo
halina ukweli,alisema Tecra.
Pamoja
na hayo Tecra anawaomba Watanzania wasamalia wema watakaoguswa wamsaidie
kwa kuwa huyu aliyempa mimba hiyo si mumewe hivyo hana msaada wowote atakaopata
wakati atakapokuwa anaendelea kuwalea watoto wake hao.
Mganga
Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Misungwi Marco Mwita aliwaambia waandishi wa
Habari kuwa tukio hili ni si la kawaida kutokea mara nyingi wakina mama
wamekuwa wakijifungua watoto watatu na si wanne kama ilivyotokea kwa Tecra.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment