Baadhi ya wananchi wilayani Geita
Mkoani Geita wamemuomba (IGP) Ernest Mangu kumrudisha aliyekuwa kamanda wa
Mkoani Geita Leonad Paulo aliyeamishiwa Mkoa wa Marogoro hivi karibuni.
![]() |
IGP ERNEST MANGU |
Wakiongea kwa nyakati tofauti,
wakazi hao wamefikia uamuzi huo kutokana na kukithiri kwa mauaji
yanayosababishwa na majambazi ambao wamefanya wakazi wa mji huu kukosa amani na
kushindwa kufanya kazi zao za kila siku kwa kuogopa kuvamiwa.
![]() |
RPC Morgroro Leonard Pul |
![]() |
RPC Geita Joseph Konyo |
Mmoja wa Mwananchi aliyejitambulisha
kwa Jina la Mashanja Juma kutoka Katoro wilayani humo, alisema kuwa wakati wa
kamanda Paulo majambazi waliisha na mauaji ya vikongwe yalipungua kwa kasi,
lakini kwa sasa vikongwe wanazidi kukatwa na kuuawawa huku majambazi wakizidi
kumaliza maisha ya ndugu na jamaa zao.
Juma aliongeza kuwa Matukio makubwa
ambayo yametokea kwa kipindi cha muda mfupi tangu kamanda Paulo aondoke
ni pamoja kuwavamia wafanyabishara wawili na kumua mmoja wao Gozibati Walwa,
ambapo walichukuwa pesa na bastola.
Alilitaja tukio la pili kuwa ni
kuteka kituo cha polisi Bukombe na kuua askari wawili ambao ni PC Dastan
Kimati(25) na Horia Mwandija(30) na
kujerui wawili, Mohamed Hassan(25
na Devis Ngutama(44) pia walibeba bunduki na mabomu
pamoja na risasi na kutokomea, japo bunduki inasemekana zimekamatwa lakini
wananchi bado wana hofu kubwa.
Wananchi wa Geita wanasema wakati wa
uongozi wa RPC Paul mkoani humo, ofisi yake ilikuwa wazi kila wakati kwa
watu wote ndio maana alipelekewa tarifa za tatizo na kulifuatilia mara moja, alisema
Juma.
Matukio ya kuendelea kuuawa kwa watu
yamezidi kuwafanya wakazi wa mji huo kutofanya kazi zao kwa uhuru, hivyo
kumuomba IGP kutenga kanda maalumu katika mkoa wa Geita, Huenda ikapunguza
mauaji.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment