MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 30 October 2014

ASKOFU ASHTUSHWA NA MAUAJI – GEITA



Na Valence Robert Geita.
WANANCHI Mkoani Geita wametakiwa kuacha mara moja  tabia ya  kuwaua vikongwe kwa imani za kishirikina na kuacha kujichukulia sheria mikononi kwani kufanya hivyo wanakwenda kinyume na mapenzi ya Mungu.

Kauli hiyo imetolewa jana na Asikofu wa kanisa la Habari Njema, Tryphone Siku, wakati wa kufungua mkutano wa siku tano katika viwanja vya shule ya msingi kalangala vilivyoko mjini hapa. Lengo likiwa ni kuwaombea watu kuacha dhambi na kumrudia mwenyezi Mungu.

Tryphone alisema kuwa watu wa Mkoa huo wamekuwa wakiwaua vikongwe kwa imani za kishirikina na kujichukulia sheria mikononi kwa kuwauwa wahalifu hivyo kuwaomba kuacha mara moja kwani wanakwenda kinyume na mapenzi ya Mungu na kuwataka, waganga wanaopiga ramli chonganishi nao kuacha.

Aliendelea kusema kuwa viongozi  wa Serikali wa Mkoa wa Geita kwa kushirikiana na mkuu wa mkoa huo Said Magalula wamekuwa wakijitahidi sana kuwaelimisha wananchi kuacha tabia hizo kwa kushirikiana na makanisa likiwemo kanisa lake.

Naye Mchungaji wa kanisa hilo Alex Mshindi kutoka Rwanda alishukuru wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye mkutano huo lakini akawaomba  wakazi wa Mkoa wa Geita kwa ujumla kuwa wanatakiwa kumrudia aliyewaumba na kuacha matendo maovu.

Nimeshangazwa na mauaji ya vikongwe  na kujiochukulia sheria mikononi ninavyosikia hapa Mkoani  kwenu jamani acheni tabia hizo lakini tushirikiane kuwaombea wanaofanya hivi waache na wamrudie muumba wao. Alisema Alex.

Na Mwanaharakati.

No comments: