MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 2 December 2014

KUUAWA WATU WAWILI PWANI, SOMA UNDANI WA TAARIFA HIYO



Polisi mkoani Pwani limelazimika kuingilia kati kutuliza kuzuka kwa mapigano kati ya wafugaji wa jamii ya Wasukuma na Wamang’ati baada ya kutokea mauaji ya watu wawili  chanzo kikiwa  ni kuibwa kwa ng’ombe 51

Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani Ulrich Matei amesema kuwa tukio hilo limetokea juzi katika eneo la Kitale tarafa ya Chole wilayani Kisarawe ambapo watu wawili wameripotiwa kufariki dunia katika tukio hilo.

Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Fatuma Kimario amethibitisha kutokea kwa mauaji ya watu wawili yaliyosababishwa na tukio la wizi wa ng’ombe uliofanywa na kijana wa Kimang’ati.

Aidha Bi Kimario amesema kuwa katika tukio hilo watuhumiwa wanne wanaendelea kuhojiwa na vyombo vya dola huku pikipiki nane zikiwa zimekamatwa baada ya kuachwa na maedereva waliokuwa wakiziendesha .

Sanjari na hayo bi. Kimario amesema kuwa hali ni shwari eneo la tukio na vyombo vya ulinzi na usalama vimetoka eneo la tukio na amelaani kitendo cha wafugaji kujichukulia sheria mkononi baada ya kumkamata na kumuua mtuhumiwa anayedaiwa kuiba ng’ombe hizo na pia upande wa pili kuamua kulipiza kisasi.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: