MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 19 March 2015

WANANCHI KATA KAGONDO MANISPAA YA BUKOBA WAKATAA KUMSIKILIZA DIWANI WAO BAADA YA KUSHINDWA KUITISHA MIKUTANO TANGU AINGIE MADARAKANI.



Diwani kata Kagondo manispaa ya Bukoba, ambaye hatahivyo alikuwa meya wa manispaa ya Bukoba Anatory Aman, amezomewa na wananchi baada ya kuitisha mkutano wa hadhara kuzungumzia matatizo ya maji yanayowakabili wananchi wa kata hiyo.

Katika mkutano huo, Mh Aman alitaka kujua undani wa matatizo ya maji yanayowakabili wananchi hao, ambao hatahivyo wameshalalamika zaidi ya mwaka sasa, tangu kujengewa kwa vyanzo mbalimbali vya maji na kusababisha ukosefu mkubwa wa maji kwa wananchi hao....................


Wananchi wameanza kumzomea diwani huyo, kwakusema kuwa yeye hafai kuwaongoza kutokana na kushindwa kuitisha mkutano hata mmoja, tangu achaguliwe kuwa diwani wa kata hiyo kwenye uchaguzi mwaka 2010.

Siku chache zilizopita, wananchi wa mtaa wa Kagondo Karuguru, alitoa malalamiko yao kuhusu vyanzo hivyo vya maji kupitia vyombo vya habari, ambapo katika mkutano huo, diwani wao alitaka kuwaeleza jinsi alivyoweka mpango wa kupeleka wataalamu ili watoe ushauri na kushughulikia tatizo hilo, ambalo limetokana na kujengewa kwa vyanzo vya asili vya maji ambavyo baada ya kujengewa kwa sementi na kuwekewa mabomba, maji yameonekana kukauka kama siyokuziba.

Katika maelezo yao wananchi, vyanzo hivyo vilijengewa na TASAF mwanzoni mwa mwaka jana, ambapo vilifanya kazi kwa muda wa wiki mbili tu.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: