MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday, 25 July 2015

ASKOFU KILAINI APIGA MSUMALI VYAMA VYA SIASA



. Asema wawaletee wagombea wanaopendwa,
. Watumiao udini, siasa na ukabila hawafai,
. Hatosita kusema kama mambo yanakwenda vibaya.

Askofu msaidizi wa jimbo katoliki la Bukoba Dr Method Kilaini, ameiambia sautiyamnyonge kuwa, kiongozi anayetakiwa na jamii ndiye anayepaswa kuchaguliwa na chama kwani wao ndiyo wapiga kura hivyo wasikoseshwe haki wanayoipendekeza kuwaongoza.

Hatahivyo ametaja sifa za kiongozi kuwa lazima wananchi wamuulize amewafanyia nini kabla, atafanya nini lakini akasema kuwa wananchi wanakosa elimu ya kutambua kiongozi bora, hivyo sautiyamnyonge ni moja ya chombo cha kuwasaidia watu hao
Kumekuwa na desturi za kusambaza kauli za ubaguzi na kusema udini katika siasa, jambo ambalo amesema haiwezekani wakaendelea kutumia majukwaa kutukana, akisistiza kuwa angeweza angemwapisha mmojammoja ili akikiuka alaniwe.

Vyama vya siasa kote nchini, vinaendelea na mchakato wa kuwapata wagombea wa nafasi ya udiwani, ubunge na urais, huku kukiwa katika mchakato wa kuomba ridhaa kupitia vyama vyao, ili apatikane kiongozi mmoja kila kata na jimbo kama ambavyo amepatikana mmoja kwenye nafasi ya urais kupitia CCM.

Katika manispaa ya Bukoba, wagombea ubunge ni wanane, ambapo wajumbe wa kata kupitia chama hicho, wamemwambia mbunge anayemaliza muda wake, kuwa asiangaike kuomba kura, na chama kingempitisha bila kupingwa ili aendelee kuleta mazuri anayowafanyia. 

Na Mwanaharakati.

No comments: