MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 17 September 2015

NEWS ALERT!!! HATIMA YA NCCR MAGEUZI NDANI YA UKAWA



. Wadai CHADEMA kimepora kila kitu cha UKAWA,
. Chasema kimeamua kupambana chenyewe,
. Wadai wameshindwa kukubaliana na mwenyekiti wao.
Makamu mwenyekiti wa NCCR Mageuzi Bi. Reticia Ghati Mosore akiambatana na katibu mkuu bara wa chama hicho Bw John Mosena Nyambabe pamoja na viongozi wengine wa juu wa chama hicho, wamesema kuwa wanaamua kupambana kivyao kwa masikitiko makubwa, baada ya kuona muda umeshakuwa mfupi, na hawawezi tena kufaidika na UKAWA kwani maelngo yao yameporwa na CHADEMA.

Wametumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi kuwasaidia kuwachagua wagombea wao 12 pekee waliopewa na UKAWA, wakisema kuwa hawana namna lakini hawako tayari kuendelea kutegemea UKAWA ambayo sasa imegeuka kuwa CHADEMA, kwani baada ya uchaguzi wameshajiona kama watashinda hawawezi kuthaminika kutokana na mwenendo uliopo sasa, wala wanaona hawawezi kupata nafasi yoyote katika serikali itakayoundwa.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: