MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday 18 November 2015

WIZARA YAPIGA MARUFUKU KULIPIA UMEME; SOMA UNDANI



. Imewataka wananchi kutokubali kuchangia fedha ili kuunganishiwa huduma ya umeme.


Msemaji wa wizara ya nishati na madini  Badra Masoud, amesema kuwa serikali haijaweka mpango wa kuchangisha watu hela kwa ajili ya huduma, afisa wa wizara wala kulipa fundi wa Tanesco, akiongeza kuwa fedha elekezi inaweza kuhitajika katika maeneo ambayo hayako kwenye mpango wa wizara kufikisha umeme kwa wakati huo.
Amesema kuwa nchi inakua kwa kasi na serikali imejipanga kufikisha umeme kila eneo kulingana fedha zinavyopatikana kwa kusisitiza kuwa kuna lawama kuhusu mgawo wa umeme, ambao amefafanua kuwa saizi haukuna mgawo ingawaje ubovu wa miundombinu ndiyo husababisha kukosekana kwa umeme kwa wakati Fulani.
Kutokana na mabadiliko ya tabia nchi duniani na uharibifu wa vyanzo vya maji,  Tanzania inakosa mvua za kutosha  na kusababisha gharama za umeme kupanda baada ya mabwawa ya Mtera kukauka ambayo huzalisha umeme wa wa bei nafuu kuliko umeme wa aina yoyote mpaka sasa.

Tanzania ina megawati 1500 za umeme ambazo hutumika kati ya megawati 800 na 900 nchi nzima kutoka vyanzo vya  Ubungo one, Tegeta, Nyakato Mwanza megawati 60, Ubungo two ya gesi na kampuni ya Symbion pamoja na IPTL na AGRECO zinazotumia mafuta, ingawa serikali inaendelea kuongeza kiasi cha umeme huo kwa kuwekeza katika gesi na makaa ya mawe.
 
Na Mwanaharakati.

No comments: