MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday 24 March 2012

 Ni baada ya wanafunzi wa ualimu mwaka wa kwanza na wa pili walipo chuoni hapo kufanyishwa kazi ngumu za kugonga kokoto karai 3 au zaidi kila jioni, pamoja na kujipikia wakti wanalipa kiasi cha shilingi milioni moja na 30 elfu.   PICHA HII CHINI NI JIWE LINALOGONGWA NA WANAFUNZI ILI KUPATA KOKOTO.
 Chini ni baadhi ya majengo ya chuo hicho ambayo hayajakamilika na ujenzi wake unaendelea lakini kazi za kubeba vifusi baada ya kushushwa na gari inafanywa na wanafunzi hao ambao wanalalamika.
 Mkuu wa chuo picha ya chini MICHAEL RWEKITI, alipozungumza nami amekili uwepo wa hali hiyo ambayo hata hivyo baadhi nimeishuhudia mwenyewe na amesema hakujua kama ni makosa pengine alijua ni shughuli ya kawaida hivyo atarekebisha.
 Mkuu wa wilaya ya BUKOBA Bwana SAMWEL KAMOTE, baada ya mimi kumfanyia mahijiano ameagiza uchunguzi ufanyike chuoni hapo ili kunusuru wanafunzi hao zaidi ya 160 ambao hata hivyo wanashinda njaa wanapokuwa BTP-Block Teaching Placties, wakati wamelipia mwaka wa kwanza elfu 75 na wa pili laki moja.
 Chini ni mkaguzi mkuu wa Shule manispaa ya Bukoba ameomba nimpe muda kwani hata hivyo amepewa maelekezo ya kukagua vyuo vilivyo chini ya VETA.
Ni Mwalimu MEDAD BISHAGAZI Afisa mkaguzi mkuu wa shule Manispaa ya Bukoba.

No comments: