MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 18 March 2012


KUTEULIWA KUWA MKUU WA JESHI LA KUJENGA TAIFA

Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Meja Jenerali Samwel Albert Ndomba  kuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa kuanzia tarehe 14 March 2012.

Meja Jenerali Samwel Albert Ndomba alizaliwa tarehe 22 Apr 1954 wilaya ya Mbinga, mkoa wa Ruvuma. Meja Jenerali Ndomba aliandikishwa Jeshi mwaka 1976 na kutunukiwa kamisheni 1977.

Katika Utumishi wake amewahi kushika madarakayafuatayo, Afisa Mnadhimu Makao Makuu ya Jeshi, Mkuu wa Wilaya Ngara, Mkuu wa Mkoa Arusha na Mkuu wa Utumishi wa Jeshi.

Meja Jenerali Ndomba anashika nafasi iliyoachwa wazi na Meja Jenerali Samweli Kitundu ambae amestaafu kwa mujibu wa sheria.

Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano,
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
SLP 92023, Simu: 0764-742161
Email:ulinzimagazine@yahoo.co.uk

No comments: