MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 8 April 2012

TASWA YAZUNGUMZIA MAMBO MATATU;

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
A.MSIBA WA KANUMBA
CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kinaungana na wasanii wote nchini na Watanzania kwa ujumla kuombeleza kifo cha msanii mahiri Steven Kanumba kilichotokea usiku wa kuamkia Jumamosi jijini Dar es Salaam.

B.PONGEZI KWA SIMBA KUINGIA 16 BORA
TASWA inatoa pongezi za dhati kwa timu ya Simba ya Dar es Salaam baada ya kufanikiwa kuingia hatua ya 16 Bora ya michuano ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kwa kuitoa ES Setif ya Algeria Ijumaa iliyopita.

Tunawasihi wachezaji wa Simba na viongozi pamoja na mashabiki wa klabu hiyo, wasibweteke na mafanikio hayo badala yake waunganishe nguvu ili waingie hatua inayofuata hatimaye watwae ubingwa maana hakuna lisilowezekana chini ya jua. 
C. WAANDISHI WALIOSHINDA TUZO
Kamati ya Utendaji ya TASWA inatoa pongezi za dhati kwa waandishi wa habari za michezo walioshinda Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari (EJAT) zilizofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Waandishi hao ni Imani Mani aliyeshinda upande wa magazeti, Anwar Mkama upande wa televisheni na Abdallah Majura upande wa redio, ambao tunaamini juhudi za kazi zao zimefanikisha kupata tuzo hizo.

Nawasilisha.

Amir Mhando

Katibu Mkuu TASWA
08/04/2012           

No comments: