MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 24 May 2012

KAMATI YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI IMEIKATAA TAARIFA YA MATUMIZI YA FEDHA ZA SERIKALI MKOANI KAGERA.

 
 Akiongea mbele ya waaandishi wa habari mwenyekiti huyo John Cheyo, amesema kamati haijaridhishwa na matumizi ya serikali yanaoishia mwezi june mwaka 2011, akifafanua kuwa miongoni mwa miradi iliyoifanya kamati kusikitika ni pamoja na usitishwaji wa mradi wa Bilioni 5.06 wa Kabanga Bay ulioasitishwa na serikali ya mkoa, akisema kuwa umeishagharimu serikali bilioni 1.7 kwa kusema kuwa mkandarasi aliyekatishiwa mkataba akiipeleka serikali mahakamani atalipwa na nani, lakini pia hasara ya bilioni 17 italipwa na nani?
 Amesema kuwa kutokana na utambulisho wa afisa Mhasibu ambaye ni katibu tawala NASORO MNAMBILA, imebainika kuwa hausiki katika baadhi ya mambo hivyo ili kujiridhisha itabidi atafutwe aliyekuwa akishika nafasi hiyo awali ambaye ni MARIA BIRIA ili kupata maelezo kamili June 1 mwaka huu.
 Jambo jingine ni matumizi ya fedha katika ujenzi wa jengo la ofisi ya mkoa kwa kiasi cha shilingi bilioni 10.8 ambazo imeonekana ni kiasi kikubwa, ikasemekana kuwa kutokana na kuwa kuna ikama kubwa ya watumishi imeonekana ni kiasi kikubwa sana hivyo inabidi litolewe maelezo.
Pamoja na hiyo Bwana Cheyo aliyeambatana na ujumbe wa kamati yake amesema hali hii inaonesha ukiukwaji mkubwa wa sheria za serikali katika matumizi ya fedha.

Naye katibu tawala mkoani Kagera Bwana Mnambila amesema kuwa wamepokea taarifa hiyo na ameahidi kuwa wataifa kazi yeye na watendaji katika serikali ya mkoa na ameahidi kutoa majibu yaliyosahihi katika mkutano utakaofanyika huko Dar es salaam ukihusisha kamati hiyo pamoja na viongozi waliokuwa mkoani kagera na mabo wapo kwa sasa.

No comments: