MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 20 May 2012

TGNP KUFANYA MAFUNZO MIKOANI.


TANZANIA GENDER NETWORKING PROGRAMME (TGNP)
P.O. Box 8921, Dar es Salaam, TANZANIA; Gender Resource Centre, Mabibo Road,
Tel. 255 022  2443205/2443286/2443450;
Mobile 255  0754 784050, 0715 784050; 0784 784050 Fax 255  022 2443244; Email info@tgnp.org ; web www.tgnp.org
 

16/05/2012
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TGNP  kufanya mafunzo ya uraghibishi mikoa mitatu
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) utafanya mafunzo ya uraghibishi ngazi ya jamii kwa  mikoa mitatu ya Shinyanga, Morogoro na Mbeya, ambapo  katika mikoa hiyo watajikita katika wilaya za  Mbeya vijijini, Morogoro Vijijini na  Kishapu. Mafunzo haya yataanza tarehe 22 – Mei 2011 – 2 June 2012.

Mafunzo hayo yana malengo ya kuwajengea wananchi uwezo wa kushiriki, kuchambua kwa kina fursa na changamoto zinazowakabili katika mazingira yao na kuyatafutia ufumbuzi  kwa kujenga vuguvugu la ukombozi wa wanawake kimapinduzi.

Matarajio ya matokeo makubwa ya  Mafunzo ya Uraghibishi  na utafiti shirikishi wa kijamii,yatawashirikisha wanawake na wanaume   walioko pembezoni  katika kutambua fursa walizonazo katika kudai au kuingizwa kwa madai  yao katika mchakato wa Katiba mpya, kudai mabadiliko ya sera, kimfumo,  na haki ya uchumi kwa makundi yaliyoko pembezoni.

Mafunzo haya pia yatawajengea wanajamii uwezo wa kushiriki ipasavyo katika mchakato wa kutoa maoni kwa Tume ya Kuratibu Mchakato wa katiba mpya, haki ya uchumi, na maisha endelevu kwa wote.

Baada ya mafunzo haya, wanajamii wataibua vipaumbele vya changamoto zinazowakumba na watajadili namna ya kukabiliana nazo wakiwa na viongozi wa serikali ngazi ya wilaya,kata na vijiji.

Mwisho TGNP itaendesha warsha  kwa wanajamii namna ya kuanzisha  na kusimamia vituo vya taarifa na maarifa katika wilaya zao ikiwa ni sehemu ya kukutana na kushirikishana uzoefu na kujadili masuala  mbali mbali zinazowakabili.
 Imetolewa na

Usu Mallya
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP

No comments: