MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 17 May 2012

KATIBU w' CHADEMA ANAYEDAIWA KUMNG'OA SIKIO MWANANCHI AMPA SIKU 14 MKUU WA MKOA WA MWANZA KUMTAKASA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

 PICHA HII IKIMWONESHA MLALAMIKAJI ALIPOINGIA OFISI KWA MKUU WA MKOA.

Abel mwesa amesema iwapo mkuu wa mkoa hatofanya hivyo kwa muda uliotajwa atamfungulia mashitaka ya udhalilishaji. Tarehe 14 kijana Lazaro Robert alifika katika ofisi za mkuu wa mkoa wa Mwanza kutoa taarifa za kung'atwa na kiongozi huyo wa CHADEMA akililaumu jeshi la polisi kushindwa kumtia nguvuni mtuhumiwa. Kutokana na madai hayo mkuu wa mkoa wa Mwanza alitoa agizo kwa polisi kumkamata mtuhumiwa wa tukio hilo ambaye aliwekwa rumande kwa siku 2

Nae Lazaro Norbet amesisitiza kufanyiwa kitendo hicho na katibu huyo wa CHADEMA wilaya ya Ilemela akisema kuwa maelezo yake ya awali yalitofautianana na kumtaja mtu mwingine kutokana na mikwara aliyopigwa kwamba iwapo atamtaja katibu huyo kuhusika basi chamoto atakiona.

Katika hatua nyingine akizungumza na vyombo vya habari jana katika ofisi Kuu ya CCM Mkoa wa Mwanza Katibu wa siasa Itikadi na Uenezi Bw. Saimon Mangelepaa amesema kuwa CCM imesikitishwa na kitendo cha kiongozi wa juu (KATIBU) wa Wilaya ya Ilemela cha kujichukulia sheria mkononi na kumfanyia kitendo cha unyama kijana Nolbert kitendo ambacho hakina budi kulaaniwa na wananchi bila kujali tofauti za kisiasa zilizopo kwa vile ni kitendo cha kinyama kwa jamii na kimeonyesha kiongozi huyo hatambui wajibu wake kwa kuvunja sheria na kujichukulia uamuzi wake binafisi ambao umemsababishia kijana huyu ulemavu wa kudumu.

No comments: